Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Posta kilichopo Kengeja kitafanyiwa ukarabati na kutumika?

Supplementary Question 1

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba kumuuliza maswali mawili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, ni lini ulikwenda kukikagua kituo hiki cha Kengeja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa imepangiwa mwaka 2024/2025, je, kwa nini tusiachane na ukarabati na badala yake tukakijenga upya kutokana na hali ya kituo hiki ilivyo? Ahsante. (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA NA HABARI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bahati Khamis Kombo, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Mheshimiwa Mbunge alivyouliza, kwamba ni lini nitaenda kukagua. Ukaguzi unafanyika kila mara, naa tuna vituo nchi nzima na tunakwenda hatua kwa hatua. Tulifanya ukaguzi Shangani, Chakechake, na tayari tumeshafanya ukarabati katika maeneo hayo na fedha zitakapopatikana tutatenga muda wa kwenda kukagua ili tuweze kukarabati kutokana na mpango wa ndani unavyoendelea.

Mheshimiwa Spika, vilevile swali la pili, badala ya kujenga tunaanza na utaratibu wa kukarabati kwanza maeneo ambayo tunayo kwa sababu tayari mahali palipo ni kwamba ndiyo maeneo ambayo yanamilikiwa na Shirika la Posta Tanzania. Baada ya kuona kwamba sasa uhitaji utabadilika na mahitaji ya watu yakawa mengi tofauti na eneo lililopo, basi tutaangalia uwezekano wa kutafuta eneo lingine ili tuhakikishe kwamba tunakidhi mahitaji ya utoaji wa huduma za posta, ahsante.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Posta kilichopo Kengeja kitafanyiwa ukarabati na kutumika?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Posta cha Dodoma ni kituo ambacho kimejengwa muda mrefu sana na hakiendani na hadhi ya makao makuu, nini mkakati wa Serikali wa kujenga kituo kipya cha posta cha kisasa ili kiendane na hadhi ya makao makuu? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA NA HABARI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumefanya ukarabati nchi nzima na kituo cha posta kikiwaki moja wapo. Pamoja na hivyo, tunaendelea na kutafuta maeneo ya kujenga vituo vingine vipya kulingana na Serikali kuingia makubaliano na Posta ya Oman. Tunaamini kabisa kwamba katika mradi huo ambao takribani milioni 100 USD zinaenda kutumika kujenga zile logistic park. Naamini kwamba kwa sababu Dodoma ndiyo makao makuu ya nchi tutaitazama na kuhakikisha kwamba inakuwa na posta ya kisasa na yenye kutoa huduma ambazo zinaendana na mahitaji ya Watanzania.