Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupitia TBA kuwajengea nyumba watumishi wa Serikali ya Muungano kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi kunipatia fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Ukweli uliokuwepo, Shirika la Nyumba la Bara halitumi fedha kupitia Shirika la Nyumba la Zanzibar hadi muda huu.

a) Je, kuna ushirikiano gani sasa ya kuliwezesha shirika la Nyumba la Zanzibar kwa kulipatia fedha kwa ajili ya kuwajengea watumishi wa bara?

b) Je, kuna mkakati gani wa ushirikiano kati ya ZBA pamoja na TBA? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyo kwisha kusema, ni kwamba nyumba za Zanzibar kwa watumishi wa umma zinajengwa chini ya Wakala wa Majengo wa Zanzibar lakini wana ushirikiano wa karibu sana kati ya ZBA pmoja na wakala wa majengo Tanzania Bara. Ushirikiano huo ni pamoja na kwamba Wakala wa Majengo Zanzibar wamekuja mara kadhaa huku Bara kujifunza namna ambavyo TBA wameweza kuendesha miradi mbalimbali happa nchini ikwemo miradi ya Dar es Salaam Magomeni quarter hapa Dodoma pamoja na mji wa kiserikali.

Mheshimiwa Spika, lakini kwa swali lake la pili ni kwa kiwango gani TBA iipatie fedha ZBA. ZBA fedha zake zinatengwa kwenye Wizara ya Ardhi, Maendeleo na Makazi kule Zanzaibar. Na kwa mwaka wa fedha ujao, kwa maelezo ya ZBA ni kwamba wametenga takribani kiasi cha shilingi bilioni 56 ili kujenga nyumba takriban 400 zitakazo jengwa kwa Zanzibar nzima kwa maana ya Unguja na Pemba, na walau kila Wilaya watagusa kupitia mradi huu.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupitia TBA kuwajengea nyumba watumishi wa Serikali ya Muungano kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa nyumba kadhaa zilizo chini ya mamlaka ya TBA hasa hapa Dodoma ni chakavu, miundombinu ya maji taka imechoka, maji ya karo na vyoo yanafurika hovyo na hivyo kuwa tishio kwa afya.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuisimamia mamlaka hii ya TBA ili kuhakikisha nyumba hizi ziko katika hali ya usalama na si tishio kwa wakazi, na hasa kwa vile wanalipwa kodi na hawakai bure?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Asha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli badhi ya nyumba za TBA hapa Dodoma ni chakavu, na nikushukuru Mheshimiwa Spika, kwamba baadhi ya watumishi wa Serikali wanadaiwa. Na kwa kuwa wanadaiwa wanakila sababu ya kulipa ili tukarabati nyumba hizi ambazo ni chakavu, ukizingatia kwamba TBA fedha zake zinakata kutoka ruzuku za Serikali lakini pia na kodi za mpangaji, inapokusanywa ndipo inapokarabati nyumba hizi za TBA, ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. JUMA USONGE HAMAD aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani kupitia TBA kuwajengea nyumba watumishi wa Serikali ya Muungano kwa upande wa Zanzibar?

Supplementary Question 3

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Uko ujenzi unaoendelea na TBA kule Temeke, tunaita Temeke quarter.

Je, Serikali mna mkakati gani wa kuwapatia nyumba wale ambao walikuwa wakiishi pale kabla ya ujenzi huu unao endelea?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy Kilave kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli pale Temeke Mwisho na Temeke quarter kuna mradi unaendelea na mradi huu tutajenga majengo takribani saba ya ghorofa yatakayo kuwa na uwezo wa kubeba familia 1,008 na kwa maana hiyo sasa wale wote ambao watakuwa ni waathirika wa maeneo

hayo pia TBA tutaona ni namna gani ya kuwafanya hawa waishi katika maeneo hayo.