Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nina swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa jengo hili la Halmashauri ya Bagamoyo limejengwa toka miaka ya 1970, na sasa hivi linavuja, nyaraka nyingi zinaloa na Mkurugenzi anapata shida kufanya kazi na wafanyakazi wake ambao wako katika maeneo tofauti tofauti: Je, Serikali haioni umuhimu katika bajeti ya mwaka huu kutuongezea pesa kuanza ujenzi huo mara moja, kwa sababu, mapato yetu ya Halmashauri ni madogo sana?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kweli jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo linalotumika sasa ni la muda mrefu. Kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, wao wenyewe Halmashauri walitenga fedha, shilingi milioni 500 kwenye mapato yao ya ndani na katika bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja vilevile wametenga tena shilingi milioni 500.

Mheshimiwa Spika, vilevile wao wameenda na mchoro ambao utatumia zaidi ya shilingi bilioni 5.34, lakini mchoro ule uliotolewa na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ulikuwa una gharama ya shlingi bilioni 2.7 tu. Kwa hiyo, inaonesha wao walikuwa wana uwezo wa kujijengea jengo lao wenyewe na kutenga hizi fedha kwa sababu walichagua mchoro wa ghorofa mbili badala ya ghorofa moja, naomba kuwasilisha.