Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza: - Je, lini Serikali itaboresha miundombinu ya Shule za Mtapa, Kanani na Wangutwa Wilayani Wanging’ombe?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Shule ya Sekondari ya Igwachanya kuna boma la bwalo ambalo limejengwa kwa nguvu za wananchi takribani miaka kumi sasa. Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo alipita akaahidi kupeleka pesa, na vilevile Mheshimiwa Bashungwa alipita tena akaahidi kupeleka pes: Je, lini mtapeleka pesa hizo zaidi ya Shilingi milioni 200 ili ziweze kukamilisha bwalo lile la Shule ya Sekondari ya Igwachanya?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Kuna Shule ya Msingi ya Saja, Usuka na Udonja, ziko kwenye hali mbaya sana, miundombinu yake ni chakavu sana: Je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha kwamba shule zile zinakarabatiwa na kuwa bora kama shule nyingine?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali lake la kwanza la boma la bwalo katika shule hii ya sekondari ambayo ameitaja Mheshimiwa Neema, Serikali itaendelea kutafuta fedha na kuweka kipaumbele katika kumalizia bwalo hili. Kama alivyosema yeye, ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Hivyo tutakaa na wataalam wetu kuona tutapata wapi fedha kuweza kwenda kumalizia mabwalo haya.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, la shule hizi za msingi ambazo ni chakavu, Mheshimiwa Mbunge amezitaja; Serikali inaendelea kufanya ukarabati wa miundombinu ya shule za msingi na ninyi Waheshimiwa Wabunge humu ndani mtakuwa ni mashahidi, kuna zaidi ya Shilingi bilioni 230 ya mradi wa boost ambayo tayari fedha zile zimeshakuwa disbursed katika shule hizi kwa ajili ya kuanza ukarabati na ujenzi wa miundombinu mipya katika shule hizi za msingi na ni nchi nzima.