Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nawashukuru sana TAMISEMI kwa kazi wanazozifanya katika Jimbo la Ushetu. Tumepokea vifaa vya meno na x-ray, lakini hatuna wataalamu wa meno na mtaalamu wa mionzi: Je, katika ajira hizi 8,000 tutapatiwa hao wataalamu wa mionzi kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa Jimbo la Ushetu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Nina Zahanati ya Bugomba A, Elias Kwandikwa, Bugera, Manungu pamoja na Makongoro, zina watumishi wawili wawili tu, inafika mahali Jumapili na Jumamosi wanafunga kwa ajili ya kupumzika. Katika watumishi hawa 8,000, na hizi zahanati zitapata watimishi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa
Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cherehani, swali lake la kwanza la wataalamu wa meno na mionzi, kwa sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ina timu ambayo inazunguka katika Halmashauri mbalimbali zilizopokea vifaa tiba kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wataalamu wetu kule kuweza kujua namna ya kutumia vifaa hivi vya kisasa vinavyokwenda. Kwa hawa wataalam wa meno na wa mionzi, tutahakikisha kwamba hospitali hii pia inapata wataalamu hawa kwenda kusaidia wananchi wa kule Ushetu.

Mheshimiwa Spika, nikijibu kwenye swali lake la pili, kama ambavyo nimesema kwenye majibu yangu ya msingi, hawa watumshi 8,070 ni katika upungufu uliopo nchi nzima, ikiwepo kule Ushetu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ushetu nayo itapokea watumishi hawa wa afya.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya Nkwenda na Hospitali ya Wilaya ya Kyerwa ina upungufu mkubwa wa watumishi. Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa tiba ili kuondoa adha wanayoipata wananchi wa Jimbo la Kyerwa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, katika hawa watumishi 8,070 ambao Serikali itaajiri hivi punde, tutahakikisha Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa nayo inapata watumishi hawa. Kwenye vifaa tiba, Serikali ilikuwa imeshatoa shilingi bilioni 34 nchi nzima katika kuhakikisha hospitali hizi za Wilaya zinapata vifaa tiba na tutaangalia pia kama hospitali ya Wilaya ya Kyerwa imo na kama haimo, basi itaingia katika mwaka wa fedha ambao unafuata.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Kata ya Ndanda wananchi walijitolea, lakini pia walishiriki na nguvu ya Ofisi ya Mbunge kwa maana ya Mfuko wa Jimbo, kukamilisha Kituo cha Afya baada ya kupata pesa Shilingi milioni 50 kutoka Serikali Kuu. Sasa hivi limebaki suala moja tu ili iweze kufunguliwa, ambalo ni choo. Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutoa maelekezo kwa DED wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi, DC, wakamilishe choo hicho ili zahanati ianze kutumika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri mbele ya Bunge lako hili kwamba Mheshimiwa Mwambe alishakuja kulifuatilia jambo hili ofisini kwa karibu kabisa. Nitumie nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha anajenga choo hiki kupitia mapato yake ya ndani ili huduma ziweze kuanza kutolewa katika kituo hiki.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na Vifaa Tiba katika Hospitali ya Halmashauri ya Ushetu?

Supplementary Question 4

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naitwa Aloyce John Kamamba.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tunaishukuru Serikali kwamba imekamilisha ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kakonko, lakini tuna upungufu mkubwa wa watumishi na vifaa tiba. Lini Serikali itapeleka watumishi na vifaa tiba katika hospitali yetu ya Wilaya ya Kakonko? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali inaajiri watumishi wa afya 8,070, na katika hawa ambao wataajiriwa, Hospitali ya Wilaya ya Kakonko nayo itapata watumishi hawa.

Mheshimiwa Spuika, kwenye vifaa tiba, vilevile Serikali imetenga zaidi ya Shlingi bilioni 34 ambazo zimeshakwenda kwa wenzetu wa MSD kwa ajili ya kupeleka vifaa tiba kwenye hospitali za Wilaya mbalimbali hapa nchini na tutaangalia kama Hospitali ya Wilaya ya Kakonko nayo ipo, kama haipo tutaiweka katika mwaka wa fedha unaofuata.