Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ameir Abdalla Ameir

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha utalii wa ndani unaimarika?

Supplementary Question 1

MHE. AMEIR ABDALLAH AMEIR: Mheshimiwa Spika,ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ningeomba kuuliza masuala mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tuna maeneo ambayo yana vielelezo vya kihistoria kati ya Tanzania bara na Tanzania visiwani yanayo shabihiana; kwa mfano hatuwezi kuzungumza biashara ya utumwa tukaielezea sehemu moja ina elezeka sehemu zote mbili wanahistoria Dkt. Livingstone.

a) Je, Wizara yako sasa inaampango gani wa kuyahuisha maeneo haya yenye vielelezo vya kihistoria vinavyotegemeana ili sasa kuusaidia utalii wetu wa ndani kukua zaidi kimapato?

Mheshimiwa Spika, kutokana na mtikisiko wa Uviko 19 tumeona kwamba utalii wetu wa ndani kidogo uliyumba;

b) Je, Wizara sasa ina mpango gani wa mikakati mipya na imara ukiachia mbali hii ya kawaida unayoelezea ya kuweza sasa kuufanya utalii wetu wa ndani uweze kujitegemea angalau kwa asilimia hamsini kwa hamsini, huku ukizingatia kwamba tunapoboresha vya kutosha Tanzania kutokana na ongezeka la watu?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ameir Abdallah Ameir, Mbunge kutoka Baraza la Wawakilishi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ipo mikakati kabambe ambayo imeshaandaliwa na Serikali kuhakikisha kwamba tunaendelea kutunza maeneo haya ya kihistoria. Moja ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kuyatunza maeneo hayo yenyewe ili lengo na madhumuni sasa tuweze kuvutia watalii wengi; lakini cha pili kuendelea kufanya utafiti kwa sababu tunachoamini kwamba bado yapo maeneo ya vivutio vya watalii inawezekana bado hatujayavumbua yakiwemo maeneo ya kihistoria ya hiyo historia utumwa na vitu vingine. Sasa kuendelea kuyatangaza, kwa sababu kuwa nayo na kuyavumbua ni suala moja lakini kuendelea kuyatangaza ili walio nje na ndani ya nchi yetu waweze kutambua wapi wanaweza wakajifunza na wakapata kujua hiyo historia.

Mheshimiwa Spika, swali lingine, ni nini sasa matarajio yetu, Matarajio yetu ni kuhakikisha kwamba tunaongeza idadi kubwa ya watalii kutoka idadi tuliyo nayo kuendelea idadi kufika hata watalii milioni tano. Lengo na madhumuni ni kuongeza sasa mapato ya nchi.

Mheshimiwa Spika, ili tuweze kufikia hayo matarajio kwanza tuhakikishe kwamba tunatoa elimu kwa wananchi ili waweze kutambua umuhimu wa utalii wa ndani, lakini cha pili kutoa huduma bora hicho tumekipanga ili lengo na madhumuni wanapo kuja kujifunza waweze kupata huduma bora.

Mheshimiwa Spika,nakushukuru.