Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga taa za barabarani eneo la Tunduru Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali; lakini pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina swali dogo moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru na kupongeza mpango wa TARURA kwamba taa hizo zilizozungumzwa zimefungwa kwenye barabara ya mtandao wa TARURA ambayo ziko pembezoni mwa mji. Lakini kuna barabara ya TANROADS ambayo inapita katikati ya mji ambapo ndipo sura ya Tunduru Mjini. Je, ni lini Serikali itatufungia taa za barabarani kwenye barabara ile ya TANROADS? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhususiana na barabara hii ya TANROADS ambayo inapita katikati ya Mji wa Tunduru, nafahamu wenzetu wa TANROADS wana mkakati wa kufunga taa katika barabara zote zinazopita katika makao makuu ya wilaya nchi nzima si kwa Tunduru peke yake kwa sababu tayari za TARURA kuanzia sasa barabara yote ya lami inayojengwa na TARURA lazima ifungwe taa; hivyo hivyo na wenzetu wa TANROADS nao wameweka mkakati huo wa kuhakikisha barabara zote kubwa zinawekewa taa.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga taa za barabarani eneo la Tunduru Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika barabara muhimu kiuchumi kutoka Kalenga kwenda Uwasa imeharibika sana eneo moja la Kiponzelo.

Je TARURA inampango gani wa dharura kuweza kutupa fedha kwa ajili ya kurekebisha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa barabara hizi ambazo zimeathirika sana kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini TARURA ilikuwa na bajeti ya bilioni 11 kwa ajili ya dharura lakini sasa wameomba fedha iweze kuongezwa kutoka bilioni 11 na kwenda bilioni 46 ili kuweza kutengeneza barabara mbalimbali nchini ikiwemo za Kalenga kule kwa Mheshimiwa Kiswaga.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafunga taa za barabarani eneo la Tunduru Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itafunga taa za barabarani katika Mji wa Kakonko?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za Kakonko anazozizungumzia Mheshimiwa Mbunge pale ni kama lilivyokuwa swali la kwanza la Tunduru Mjini ni barabara ya TANROADS na tayari ni mkakati wa TANROADS kuhakikisha kwamba wanafunga barabara katika barabara zote zinazopita makao makuu ya wilaya, na hivi karibuni zoezi hilo litaanza.