Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Duma Bariadi Mkoani Simiyu?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Nimuulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa daraja la Mto Tungu ni muhimu sana Wilaya ya Maswa, inaunganisha Maswa na Kishapu.

a) Je, ni lini Serikali itatenga pesa za kujenga daraja hilo?

b) Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Sandai, Wilaya ya Itilima kwenda Hospitali ya Wilaya ya Nkolo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kipaumbele cha Serikali kupia TARURA kuhakikisha kwamba barabara zote zinazounga wilaya na wilaya zinapata huduma bora ya barabara, na barabara hii ambayo Mto Tungu umepita inayounganisha Wilaya ya Kishapu na Maswa nayo itatengewa fedha kwa ajili ya kuweza kujenga daraja hii ili iweze kupitika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali lake la pili la barabara ya Saadaye-Nkolo, hii barabara inaelekea katika hospitali kama sikosei nimeshawahi kupita maeneo hayo, na ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inatengenezwa vilevile ili wananchi waweze kuapata huduma ya afya katika hospitali ya mission iliyokuwepo kule. Kwa hiyo tutatenga fedha kuhakikisha kwamba barabara hii inatengenezwa.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Duma Bariadi Mkoani Simiyu?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je ni lini Serikali itajenga Daraja la Unguuni katika Kata ya Nduruma ambayo imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na TARURA na sasa wananchi wanateseka hasa katika kipindi hiki cha mvua na mafuriko yanayowasumbua wananchi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, daraja hili la Kata ya Nduruma tutaangalia kama lipo kwenye bajeti ya mwaka huu ambayo imeshapitishwa lako Tukufu kwa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA). Kama haipo basi tutahakikisha inatengewa fedha katika mwaka wa fedha unaofuata.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Duma Bariadi Mkoani Simiyu?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa. Ni lini Serikali itajenga daraja la kutoka Itununu kwenda Igodi kafu ambayo ni Jimbo la Isimani kuhakikisha kwamba wananchi wanaweza wakapata huduma ya kwenda kwenye Hospitali ya Wilaya na wanafunzi wanashindwa kwenda shule?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itajenga barabara hii ya Itununu kwenda Igodi Kafu kadiri ya upatikanaji wa fedha. Na kwa sababu kuna huduma muhimu kama ya shule na vilevile kituo cha afya ambapo wananchi wanapata huduma basi tutaiangalia na kuiwekea kipaumbele ili barabara hii nayo iweze kutengenezwa.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Duma Bariadi Mkoani Simiyu?

Supplementary Question 4

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Ni lini Serikali itatoa fedha kujenga Daraja la Mto Ruvuma kati ya Lusomba -Magabula kwa Mheshimiwa Jenista Mhagama hadi Iyale ambapo Mheshimiwa Jenista tumehangaikia sana hili daraja?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itajenga daraja hili la Lusonga hadi Liyanja kadri ya upatikanaji wa fedha; na tutaangalia kama imetengewa fedha katika mwaka huu wa fedha ambao tumepitishiwa ili tuweze kwenda kuweka kipaumbele katika daraja hili ili wananchi waweze kupata huduma hiyo.