Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaimarisha ulinzi na usalama wa maeneo ya maziwa na bahari ili kulinda rasilimali pamoja na wavuvi?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa mpaka sasa wavuvi wetu wameendelea kupigwa na kunyang’anywa mali zao hasa malighafi ya samaki maeneo ya ziwani. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuimarisha Jeshi la Marine Sota pale Wilaya ya Rorya ili kuimarisha ulinzi maeneo ya ziwa kwa ajili ya kulinda wavuvi pamoja na malighafi Samaki?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa zoezi hili la uhalifu linafanywa na askari wa nchi jirani. Serikali haioni umuhimu sasa kupitia Wizara kufanya mazungumzo na nchi hizi jirani ambao wanafanya uharibifu na kupiga wavuvi wetu ili waweze kuacha zoezi hili mara moja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uimarishaji wa Kituo cha Marine Sota, nadhani nikubali hiyo ahadi. Mwezi uliopita Waziri wangu alitembelea eneo hilo na ile ilikuwa ni moja ya concern kwamba Kituo cha Marine cha Sota kiko dhaifu. Kwa hiyo kupitia hadhara hii ya Bunge lako tukufu, nimwombe Mkuu wa Jeshi la Polisi azingatie kuimarisha Kituo hiki cha Sota ili kiweze kutimiza wajibu wake ipasavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu uhalifu kufanywa na wanaodhaniwa kuwa ni askari wa nchi jirani, Jeshi la Polisi litafanya uchunguzi, pale itakapothibitika tutaimairisha vikao vya ujirani mwema kati ya wakuu wetu wa vyombo kudhibiti suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.