Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya kutoka Geita – Bukoli hadi Kahama?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; je, nini upi mpango wa Serikali katika ujenzi wa barabara ya Katoro – Kaseme – Magenge hadi Ushirombo?

Swali la pili; ni lini Serikali itapandisha kiwango cha barabara kutoka Geita – Buyagu – Kamena hadi Bukoli ili iweze kuhudumiwa na TANROADS ukizingatia kwamba maombi yake yamekwishafikishwa Wizarani? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Katoro – Ushirombo imeshakamilishwa kufanyiwa usanifu, sehemu ya barabara hii pia tunao mradi wa RISE ambao kipande fulani kitatekelezwa kwenye mradi wa RISE ambao taratibu za manunuzi zinaendelea wakati Serikali inatafuta fedha kukamilisha barabara yote ya Katoro – Nyikonga hadi Ushirombo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la barabara ya Geita – Nyankumbu – Kamena hadi Bukoli nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama imeshaletwa kwenye Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa ajili ya kupandishwa hadhi, Serikali itaangalia kama inakidhi vigezo ili barabara hii iweze kupandishwa hadhi na iweze kusimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya kutoka Geita – Bukoli hadi Kahama?

Supplementary Question 2

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuendeleza barabara ya Kiluvya – Kisarawe ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inaiunganisha Wilaya ya Kisarawe na Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira tuone kwenye bajeti tunayotegemea kuileta mbele ya Bunge lako kama itakuwa na hiyo barabara. Nimhakikishie Mheshimiwa Serikali inatambua umuhimu mkubwa sana wa hiyo barabara kuijenga kwa kiwango cha lami.