Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, ni lini changamoto ya maji ndani ya Jimbo la Momba litatatuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kuwa muwazi na kukiri kwamba tunayo changamoto ya maji kwenye Jimbo la Momba. Nitauliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Serikali inawasilisha mpango wa bajeti hapa walisema upatikanaji wa maji vijijini ni asilimia 78, na Mheshimiwa Waziri amekiri hapa kwamba tunayo adha ya maji; je, kwa kuwa anaenda kuanzisha Mradi wa Mto Momba, ipi commitment yake kwamba, mwaka wa bajeti unaokuja nasi tutafikia asilimia 78 kama wenzetu wa vijijini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Tarehe 11 Novemba, 2022 Mheshimiwa Rais wakati anazindua vifaa vipya vya kisasa vya uchimbaji, yapo maneno kadhaa ambayo alimweleza Mheshimiwa Waziri, nami sitaki kuyarejea, kwani anakumbuka, kwamba hatavumilia kuona wataalam wanaendelea kusema wamefanya utafiti na hawajaona maji. Momba hayo mambo yanaendelea, kila wakienda kufanya utafiti hawaoni maji: Ipi kauli ya Mheshimiwa Waziri kudhibitisha yale maneno ya Mheshimiwa Rais siku ya tarehe 11 Novemba, 2022?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyowapigania wananchi wake wa Momba. Maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kwamba tunakwenda kutumia rasilimali toshelevu kwa ajili ya kutatua matatizo ya maji. Vivyo hivyo sasa tunakwenda kutumia Mto Momba kwa ajili ya kutatua tatizo la maji Momba, na maji yale yatakwenda mpaka Tunduma ili wananchi wale waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni juu ya suala zima la utafiti. Nikiri miaka ya nyuma tulikuwa na changamoto juu ya vitendea kazi. Mheshimiwa Rais ametupatia fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kisasa ambavyo vitaweza kufanya tafiti na kuhakikisha rasilimali za maji zilizokuwa chini ya ardhi zinatumika na kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya majisafi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba hata yale magari ya Mheshimiwa Rais ambayo tumeyapata katika kila mkoa, hivi ninavyozungumza lipo katika Jimbo lake la Momba katika kuhakikisha tunachimba visima na wananchi wake wanapata huduma ya majisafi na salama. (Makofi)