Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA K.n.y. MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Pamoja na kutengewa fedha, shilingi milioni 900 hali ya hospitali ile ni mbaya na fedha hiyo ni ndogo. Serikali iko tayari kuwaahidi wananchi wa Handeni Mjini kwamba itaendelea na utaratibu wa kupoteza fedha hizi kila mwaka ili hospitali hii ifanyiwe ukarabati yote? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi wa Handeni Mjini, kama walivyo wananchi wa Korogwe Vijijini, wamejenga sana zahanati, maboma yamesimama na hayajakamilika; Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inayamalizia na kuyakamilisha maboma yote ya zahanati nchini ambayo wananchi wameyajenga?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza, la kwanza kwamba fedha ni ndogo; fedha hii inatengwa na Serikali kuhakikisha wanafanya ukarabati wa yale majengo ambayo yalikuwepo toka zamani. Kwa mfano, nikisema kwenye Hospitali hii ya Handeni Mjini, wao walitaka kujenga hospitali mpya kabisa ya wilaya, lakini fedha iliyotengwa ilikuwa ni kwa ajili ya ukarabati wa majengo yaliyopo. Tutaendelea kutafuta fedha na kuhakikisha kwamba tunaendelea kupeleka fedha kwenye Halmashauri hizi kwa ajili ya ukarabati zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la kumalizia zahanati, nyote ni mashahidi humu ndani, katika majimbo yetu na Halmashauri zetu, Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imekuwa ikileta fedha shilingi milioni 50 za kumalizia zahanati na tutaendelea kutafuta fedha, na kadri ya upatikanaji wa fedha hizo basi tutaendelea kuleta katika majimbo hayo kuweza kumalizia zahanati ambazo zimejengwa kwa nguvu ya wananchi.