Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA K.n.y. MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga chuo cha VETA Wilaya ya Buchosa?

Supplementary Question 1

MHE. BONIVENTURE D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni miezi miwili sasa tangu fedha hizi zitumwe kule Buchosa. Je, Serikali inaweza kuwaambia wananchi ni lini mkandarasi ataanza kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa milioni 45 ni awamu ya kwanza, je, fedha zilizobaki zitatumwa lini ili kuendelea kutekeleza mradi huo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tulipeleka milioni 45 kwa ajili shughuli za awali ambazo zilikuwa kwa ajili ya due technical survey, topographical pamoja na ile ESIAM na tayari shughuli hizi zimekwisha fanyika. Mchakato uliokuwa unaendelea ni kwa ajili ya kutafuta mafundi pamoja na wazabuni wa vifaa mbalimbali kwa sababu utaratibu tutakaotumia katika ujenzi ni ule utaratibu wa force account.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tulikuwa tunaendelea na mchakato huo na hivi sasa mchakato umekamilika, tumekwisha pata mafundi wote kwa ajili ya ujenzi. Lakini vilevile tumepata wazabuni wa kupeleka vifaa eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, fedha zote kwa ajili ya ujenzi tayari ziko wizarani na kwa awamu ya kwanza tunapeleka jumla ya milioni 300 kwa ajili ya kuandaa misingi ili baadae tuweze kupeleka fedha nyingine kwa ajili ya sehemu ya juu ya majengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie tu nimuondoe wasiwasi hatutatumia mkandarasi na badala yake tutatumia mafundi kwa sababu tunatumia force account na fedha sasa hivi tunavyozungumza milioni 300 tayari iko Buchosa ili kuendelea na ujenzi wa misingi ya majengo yote tisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.