Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha kila Kata inakuwa na Mahakama hasa maeneo ya Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na ninapongeza kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ninaomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuunda hii Tume ya Hakijinai lakini moja kati ya mambo ya msingi ambayo Hakijinai itakwenda kuyafuatilia na kuyaona ni kuhakikisha kwamba huduma za kimahakama kwa maana ya huduma za kisheria kwa wananchi zinasogezwa.

Swali la kwanza, Kata ya Mwakipoya, Masanga, Lagana, Bunambiyu na Mwasuge ni Kata ambazo ziko pembezoni na ziko mbali na maeneo ya huduma ya kisheria. Sasa ni nini mpango wa Serikali walau wa kusogeza huduma hizi kujenga katika Kata hizi muhimu hizi Nne? (Makofi)

Swali la pili, huduma hizi za kisheria ni za muhimu sana na Halmashauri ama Wilaya ya Kishapu haina Mahakama ya Wilaya. Ni lini Serikali inakwenda kujenga Mahakama ya Wilaya katika Wilaya ya Kishapu? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipa nafasi nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Mheshimiwa Mbunge amependa kufahamu mpango wa Serikali katika kujenga Mahakama katika kata ambazo amezitaja. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Butondo kwamba tumeshaanza kama Serikali, na mwaka huu wa fedha tumetenga Shilingi bilioni 57 kwa ajili ya kujenga Mahakama 60 za mwanzo nchini. Kwa hiyo, kata zake alizozitaja Mhehsimiwa Butondo zitafikiwa.

Mheshimiwa Spika, swali lake pili ametaka kufahamu kama tuna mpango wa kujenga Mahakama katika Wilaya ya Kishapu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pia, katika mwaka huu wa fedha, bajeti hii ambayo tulileta katika Bunge hili, kati ya Mahakama 24 za Wilaya ambazo tunazijenga kwa zaidi ya shilingi bilioni 31 na Mahakama ya Kishapu ipo, kwa hiyo itajengwa. (Makofi)