Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Serikali imeshaweka Mkandarasi ambaye kwa sasa yuko site anaendelea na kazi ya Mradi wa umeme katika Vijiji vya Mawande-Utengule, Luhota, Ngamanga, Ikwata, Mlowa, Mkolanga, Ibumila, Mahongole, Manga Usetule, Kifumbe, Mtanga, Kitandililo, Ibatu, Nyamande, Mtulingala na Mbugani; Je, ni lini mradi huo wa umeme katika vijiji hivyo utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, niishukuru Serikali kwa mpango mzuri ambao sasa unatupa matumaini. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa, suala hili limechukua muda mrefu wa mradi huu wa REA na wa Songea na wa Makambako kwenda Songea ambao ulikuwa unaunganisha Kijiji cha Lyamkena na Kiumba. Je, ili kuwapa matumaini wananchi wangu kwa sababu suala hili kama nilivyosema limechukua muda mrefu, Waziri sasa atakuwa tayari baada ya kwisha Bunge tuende tukafanye mkutano atuambie kwamba alivyosema Machi mradi unaanza?
Swali la pili, kutoka ofisi ya TANESCO pale Makambako, kuna mita kama 400 hivi 500 kwenda kwenye Kijiji au Mtaa wa Kivavi na Mtaa wa Kibagange. Tunashukuru Serikali mlishatupa transfoma na nguzo zilianza kujengwa ni muda mrefu sasa zimesimama tumekwama nguzo za kumalizia na wire. Serikali itakuwa tayari sasa kutupa wire na nguzo ili tumalizie mradi huu wananchi waweze kufaidika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa nakubaliana na yeye na kwa ridhaa yako, baada ya Mkutano huu tutafuatana mimi na yeye kwenda kwenye maeneo yake kuhakikisha kwamba maeneo yake yanapata umeme uhakika.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, vijiji alivyovitaja kwa kweli vina urefu siyo mrefu sana kutoka umeme unapoishia na kwa kweli kuna transfoma ya zamani pamoja na nguzo zilizooza, kwa sasa tunafanya mabadiliko ya kubadilisha transfoma kwenye maeneo yake. Mabadiliko haya yatajumuisha pia vijiji vya Mheshimiwa Mbunge alivyouliza, kadhalika Mheshimiwa Mbunge nikuhakikishie kwamba katika ziara yangu kwenye swali lako la nyongeza la kwanza. Napenda niunganishe na vijiji vyako hivyo viwili nitavitembelea ili kuona kama hizo transfoma zilizopo zinafaa au hazifahi ili tufanye marekebisho.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Serikali imeshaweka Mkandarasi ambaye kwa sasa yuko site anaendelea na kazi ya Mradi wa umeme katika Vijiji vya Mawande-Utengule, Luhota, Ngamanga, Ikwata, Mlowa, Mkolanga, Ibumila, Mahongole, Manga Usetule, Kifumbe, Mtanga, Kitandililo, Ibatu, Nyamande, Mtulingala na Mbugani; Je, ni lini mradi huo wa umeme katika vijiji hivyo utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza naomba niipongeze sana Serikali kwa kazi nzuri sana inayofanya ya kusambaza umeme kupitia REA, REA I, REA II na REA III kwa sasa. Swali langu kwa sababu kuna vishoka wamejitokeza ambao wanaharibu sifa nzuri ya TANESCO, wanaojifanya kwenda kutandaza nyaya kwenye nyumba za watu lakini wanachukua pesa zao halafu hawa hawarudi tena kwa ajili ya kusambaza huo umeme. Je, Serikali inaweza ikawaagiza Mameneja wa Kanda, Mameneja wa Mikoa, Mameneja wa Wilaya ili kusudi waende wawabaini hao vishoka wasiwaibie wananchi hasa katika Jimbo la Sumve?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kati ya wahudumu wanaotoa huduma kwenye Shirika la Umeme kuna wafanyakazi wengine wala siyo wa TANESCO ni wafanyakazi bandia ambao wanaitwa vishoka. Pamoja na Wabunge mnaonisikiliza nichukue nafasi hii tu kuwatahadharisha kwamba wafanyakazi wa Mashirika ya Umeme Tanzania ni wafanyakazi ambao wanafanyakazi kwa maadili ya utumishi wa umma. Hata hivyo, tunatambua inawezekana wapo wachache kati yao ambao pia wanashirikiana na vishoka kuhujumu nguvu umeme ya TANESCO.
Mheshimiwa Spika, kwa sasa hivi tumechukua hatua makusudi tumeanza kuwabaini wale Mameneja ambao wanashirikiana na vishoka tumeshaanza kuwa-identify na mpaka sasa kuna vishoka takribani 19 wamekamatwa na naomba sana nitamke hili na kuanzia sasa ofisi zetu zote za Kanda pamoja na Mikoa wale Makandarasi wanaohusika kuunganisha nyaya kwenye nyumba wanaorodheshwa kwenye ofisi zetu.
Kwa hivyo basi, kama kutakuwa na wakandarasi ambao hawapo kwenye orodha ya ofisi zetu hao ni vishoka na hawakubaliki. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niongeze kwenye jibu hilo, hadi sasa Shirika la Umeme TANESCO limeshaanza kuchukua hatua kwa watumishi wake wasio waadilifu, hadi sasa watumishi 12 wamesimamishwa kazi kwa sababu ya kuhujumu miundombinu ya TANESCO pamoja na kushiriki kwenye kuwaunganishia umeme watu kwa njia ya vishoka.

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Serikali imeshaweka Mkandarasi ambaye kwa sasa yuko site anaendelea na kazi ya Mradi wa umeme katika Vijiji vya Mawande-Utengule, Luhota, Ngamanga, Ikwata, Mlowa, Mkolanga, Ibumila, Mahongole, Manga Usetule, Kifumbe, Mtanga, Kitandililo, Ibatu, Nyamande, Mtulingala na Mbugani; Je, ni lini mradi huo wa umeme katika vijiji hivyo utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa, swali hili linafanana kabisa hali ilivyo na katika Wilaya ya Mkalama, mkandarasi yuko site lakini aliondoka kwa muda mrefu sasa ndiyo amerudi je, mradi huu utakamilika lini wa usambazaji umeme?
Pia kuna kata nyingi ambazo hazikupitiwa na mradi huu, Kata ya Kikonda, Kinankundu, Msingi, Pambala na Mwanga, je, lini vijiji vilivyopo kwenye Kata hizi vitajumuishwa katika mradi huu?

Name

Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, mbali na majibu mazuri ya Naibu Waziri naomba nitoe ufafanuzi ufuatao, tarehe 6 na tarehe 7 mwezi huu tunafanya tathmini ya REA Awamu ya Pili, kwa hiyo, REA watakuja na orodha ya miradi iliyokamilika REA Awamu ya Kwanza, REA Awamu ya Pili tunataka na Wakandarasi tujue waliopewa kazi, malipo waliyopewa na kazi inakamilika lini. Kwa hiyo, ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania vuteni subira baada ya hiyo tathmini mimi na Naibu Waziri na Katibu Mkuu na Manaibu Katibu Wakuu tutasambaa nchi nzima kwenda kuthibitisha tuliyoambiwa kwenye kikao chetu ambacho tutakifanyia Mtera.
Mheshimiwa Spika, baada ya hapo REA awamu ya tatu inatayarishwa, lakini REA awamu ya tatu haitaanza wala orodha haitakamilika mpaka kwanza REA awamu ya pili ikamilike na turidhike kwamba imekamilika. Kwa hiyo, Waheshimiwa Wabunge tukiwa huko naomba ushirikiano wenu na ambaye anaona REA awamu ya pili haijaenda vizuri ni vizuri sana anipatie orodha kabla ya kikao chetu cha tarehe 6 na tarehe 7. (Makofi)