Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itapunguza tatizo la upungufu wa walimu katika Shule za Sekondari Babati Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na ninashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa wako walimu wanaojitolea kwa muda mrefu katika Shule ya Sekondari ya Wilaya ya Babati: Je, katika ajira mpya, Serikali iko tayari kuwapa kipaumbele hao wanaojitolea?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa kati ya shule 38, kuna shule sita ambazo zina mwalimu mmoja mmoja wa kike wa Shule za Sekondari ya Taraget, Burunge, Nar, Kameri, Ndeku na Endamanang’; je, Serikali iko tayari kuongeza walimu wa kike katika shule hizi? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la kwanza la Mheshimiwa Sillo la wale ambao wanajitolea; katika ajira hizi ambazo nimezitaja, Serikali imetoa 13,390, tutakwenda kwa kuangalia vigezo, kwa sababu ajira hutolewa kwa usawa.

Hao wanaojitolewa kama wameomba ajira hizi na wanakidhi vigezo vilivyowekwa katika tangazo la ajira, basi nao pia watapata, lakini hakutakuwa na upendeleo maalum ambao utatolewa kwa wale tu wanaojitolea kwa sababu wanajitolea, ili kutoa fursa sawa kwa wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la upungufu wa walimu wa kike katika shule ambazo Mheshimiwa Sillo amezitaja, hili agizo lilishatolewa kwa Makatibu Tawala wote wa Mikoa Tanzania kuhakikisha wanafanya msawazo wa walimu katika mikoa yao. Sasa katika ajira mpya hizi zinazokuja, kuna walimu wa kike nao wataajiriwa, wakifika mikoani kule wapangiwe katika shule zenye upungufu wa walimu wa kike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie tena hapa kuelekeza Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara kuhakikisha anafanya msawazo katika shule ambazo amezitaja Mheshimiwa Sillo kupeleka walimu wa kike kutoka ndani ya Mkoa wake.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itapunguza tatizo la upungufu wa walimu katika Shule za Sekondari Babati Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa kuna upungufu mkubwa wa walimu katika Shule za Msingi na Sekondari katika Mkoa wa Simiyu: Je, ni lini Serikali itatuletea walimu wa kutosha?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokuwa nimeshasema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali imetangaza ajira 13,390 na kipaumbele pale watakapokuwa wanapangiwa shule walimu hawa, ni kwa mikoa ile yenye upungufu mkubwa, ukiwemo Mkoa wa Simiyu.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itapunguza tatizo la upungufu wa walimu katika Shule za Sekondari Babati Vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Katika ajira mpya ambazo zinaendelea sasa, Serikali ina mpango gani kupeleka walimu katika shule mpya sita; Shule ya Sekondari Kimusi, Nyagisya, Barata, Inchugu na Nyanungu pamoja na Kubiterere ili watoto wetu waweze kusoma, na shule hizi zimejengwa na nguvu ya wananchi? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ajira mpya hizi ambazo Serikali imetoa, tutaangalia maeneo yenye upungufu ikiwemo shule hizi za Kimusi, Nyagisya, Nyamongo, zilizopo kule Tarime na Mkoa mzima wa Mara kwa ujumla.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL B. SILLO aliuliza: - Je, lini Serikali itapunguza tatizo la upungufu wa walimu katika Shule za Sekondari Babati Vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba tu kumwuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa sababu ni muda mrefu hapo nyuma ajira zilikuwa hazijatoka na kuna vijana wengi waliomaliza elimu zao toka mwaka 2014, 2015 mpaka sasa: Ni nini kauli ya Serikali kwamba baada ya kuwa mmetangaza ajira hizi 13,000 na kuwapa kipaumbele waliokuwa wame-graduate mapema zaidi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tangazo la ajira ambalo Serikali imetoa kupitia Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa walimu 13,390 imewekwa pale kwamba wale wa 2015 ndiyo wataanza kuingia, watakuja wa 2016 wa 2017 ili wasikae muda mrefu baada ya kuwa wamemaliza masomo yao ya ualimu. (Makofi)