Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itaipandisha hadhi Zahanati ya Solwa kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Kwa kutambua kwamba Solwa inahudumia watu karibia 31,000 na imebeba jina la Jimbo la Solwa; napenda kujua, Mganga Mkuu atatumia siku ngapi kumaliza ukaguzi huo? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na sehemu nyingine wamekuwa wakijitolea kuongeza majengo ya zahanati ili yaweze kuwa vituo vya afya ili kukidhi huduma, sasa napenda kujua, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba zahanati zote ambazo zinakidhi na zimeshaongeza majengo, zitabadilishwa kuwa vituo vya afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ni siku ngapi zitachukuliwa kwa ajili ya ukaguzi huu wa Zahanati ya Solwa ambayo inahudumia watu 31,000 katika Jimbo la Solwa, nitoe agizo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja, taarifa hii iwe imefika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kuona zahanati hii inaanza mchakato wa kupandishwa hadhi na kuwa kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la Mheshimiwa Dkt. Mnzava kwamba wamejenga zahanati nyingi katika maeneo ya kimkakati, ni lengo la Serikali kuhakikisha kwamba zahanati hizi ambazo zimejengwa kwa nguvu ya wananchi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu ya Tanzania, siyo Shinyanga peke yake kwamba zinapatiwa fedha na kuweza kuwa upgraded yale kwa yale maeneo ya kimkakati, na Serikali itafanya hivyo kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itaipandisha hadhi Zahanati ya Solwa kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Wananchi wa Kata Kilimilile wamejenga zahanati kwa nguvu ya wananchi na wafadhili na hiyo zahanati ina majengo ya wodi ambazo hazitumiki kwa sababu hadhi ya zahanati hairuhusiwi kulaza wagonjwa: Je, sasa ni lini Zahanati hiyo ya Kata ya Kilimilile itapandishwa hadhi ili iweze kutoa huduma katika Kata za Mabale na Kilimilile kwa wananchi hao? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchukua nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera kufika katika Zahanati ya Kilimilile katika Kata ya Kilimilile kufanya tathmini na kuona yale majengo ambayo yamejengwa kama yanakidhi vigezo vya kuweza kupandisha zahanati hii kuwa kituo cha afya na taarifa hii kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Naye nampatia mwezi mmoja ili iweze kuwa imefanyika tathmini hii.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itaipandisha hadhi Zahanati ya Solwa kuwa Kituo cha Afya?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kata ya Msaada kuna jengo ambalo lilikuwa likijengwa kwa mpango wa MAMM tangu mwaka 2008 mpaka leo halijakamilika. Naomba kujua, ni lini Serikali itamalizia jengo hilo, ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni kuhusu Kata ya Msaada, Serikali itamalizia jengo la Msaada hapa kadri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika mwaka wa fedha huu ambao umeshapitishwa na Bunge lako Tukufu, kuona kama kuna fedha imetengwa kwa ajili ya Msaada lakini kama haipo, basi tutatenga fedha kwenye mwaka wa fedha 2024/2025.