Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaowaongezea posho Madiwani?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa baadhi ya halmashauri malipo au stahiki za Madiwani zinapishana sana mathalani malipo ya simu kwa wenyeviti wa halmashauri na kadhalika, je, nini kauli ya Serikali katika hili? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, aina za posho za Madiwani zimeainishwa ambazo ziko wazi. Posho ya kwanza, ni posho ile ya mwezi ambayo nimetoka kuitolea majibu katika swali la msingi. Posho ya pili, ni posho ya madaraka ambayo posho hii pia inatolewa kwa mujibu wa waraka wa viwango vya posho vya Serikali. Posho ya tatu ni posho ya kuhudhuria vikao na posho ya kujikimu na safari mbalimbali za ndani ya halmashauri husika na nje ya halmashauri husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hizi posho za ndani zinategemeana na uwezo wa halmashauri husika. Kwa hiyo, hili tutaendelea kuwaasa wakurugenzi wa halmashauri mbalimbali nchini kuangalia walau wanatenga posho ya mawasiliano na kadhalika kulingana na uwezo wa mapato yao wenyewe ya ndani.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaowaongezea posho Madiwani?

Supplementary Question 2

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nilikuwa nataka niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza; kwa kuwa hawa Madiwani kwa muda mrefu sasa na hasa sisi wa Chama cha Mapinduzi wakati tunapokuwa kwenye kampeni za uchaguzi huwa tunasema kuna mafiga matatu kwa maana ya Madiwani, Wabunge na Rais na wao ndio wanaosimamia miradi ya Serikali. Sasa hatuoni kuna haja kwa kweli ya kuwaongeza kiasi fulani angalau kutoka kwenye eneo walipo ili kufika eneo wanalolitaka wao kwa sababu eneo ni kidogo sana? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili; hawa Madiwani kwa muda mrefu sasa huko nyuma wengi wamechaguliwa na hawapati mafunzo ya Serikali. Lini sasa Serikali itaandaa mafunzo kwa Madiwani ili na wenyewe wawe na uelewa wa kusimamia miradi yetu katika maeneo yetu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la kwanza la nyongeza la kuhusu kuongeza posho hizi za Madiwani, Serikali itafanya tathimini na kuangalia ni namna gani hili linaweza likatekelezeka kulingana na bajeti ambayo Serikali inayo. Kwa sbabu haya mambo yanahusisha ongezeko la matumizi kwa Serikali. Tayari kama ambavyo mnafahamu Waheshimiwa Wabunge wote humu ndani kwamba mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilichukua jukumu kutoka kwenye halmashauri zote la kulipa hizi posho kwa mwezi zilienda Serikali Kuu. Kwa hiyo, tutaliangalia na lenyewe na kuona kama uwezo wa Serikali utauhusu kwenye bajeti zijazo tuweze kulichukua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukienda kwenye swali la pili la mafunzo kwa Madiwani; hili liko kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zenyewe. Kuna halmashauri ambazo zinatoa maunzo haya kwa kushirikisha Taasisi za Uongozi Institute, kwa kushirikisha Taasisi kama Chuo cha Utumishi wa Umma. Kwa hiyo, niwatake wakurugenzi katika halmashauri mbalimbali nchini kuhakikisha wanatenga bajeti ya kutoa mafunzo kwa Madiwani wa halmashauri zao.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE K.n.y. DEO K. SANGA aliuliza: - Je, lini Serikali itaowaongezea posho Madiwani?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya watu muhimu sana ni Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji na Mitaa; hawa ni watu ambao wanapata posho kama ni posho inakuwa ni ndogo sana. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha watu hawa ambao ni muhimu wanaongezewa posho kubwa itakayowasaidia utendaji wao wa kazi uwe mzuri katika halmashauri zetu, vitongoji na vijiji?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwisha sema hapo awali kwamba posho hizi zinategemeana na bajeti ya Serikali na uwezo wa makusanyo ya Serikali, lakini upo waraka maalum na Sheria katika Sheria ya Serikali za Mitaa ambayo inazitaka Mamlaka za Serikali za Mitaa kote nchini kutenga fedha kwa ajili ya posho za Wenyeviti wa Vitongoiji, Wenyeviti wa Mitaa na Wenyeviti wa Vijiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, nitumie tena nafasi hii mbele ya Bunge hili tukufu kuwataka Wakurugenzi wa Halmashauri kutenga posho hizi za Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Mitaa na Wenyeviti wa Vitongoji kwa mujibu wa Sheria ile ya Serikali za Mitaa, Sura 290.