Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni changamoto gani mpya za Muungano zimejitokeza?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ya kutia moyo lakini pia nimpongeze Rais, Samia na Rais Mwinyi, kwa kutatua kero za Muungano hadi hadi kufikia 22 na kubakia kero nne. Swali langu ni kwamba kuna kauli gani ya Serikali juu ya kutatua hizo kero nne zilizo baki?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; Serikali imejipanga vipi kwa ajili ya utoaji elimu juu ya suala la Muungano kwa vizazi vijavyo? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwanza zinaendeleza ushirikiano ama zitaendeleza ushirikiano wa kuhakikisha kwamba changamoto zote zinazogusa kwenye Muungano zinatatuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukasema kwamba ili kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto hizi, ziko Kamati ambazo zimeundwa au iko Kamati ya majadiliano ya pamoja ambayo ndio inayosimamia utatuzi wa changamoto hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa kwamba pamoja na kwamba zipo changamoto zilizobakia lakini kwa kushirikiana na kamati hii tunakwenda kumaliza changamoto zote ili Muungano wetu huu saa uwe imara na uweze kudumu kwa muda mrefu. Kwa maana kwamba kuna Kamati za wataalam, Kamati za Makatibu Wakuu, Kamati za Mawaziri lakini kuna Kamati za Viongozi wakuu ambao hukaa kwa ajili ya kutatua changamoto hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa nimwambie Mheshimiwa kwamba baada ya kuwa tumetatua changamoto hizi, kinchofuata sasa ni kuwajulisha na kuwaeleza wananchi hatua tuliyofikia kama Serikali. Tumeanza na vyombo vya habari kuwaelimisha wananchi juu ya changamoto zilizokuwepo na zilizobakia. Kingine tumetoa tovuti maalumu www.vpo.go.tz wananchi wakienda hapo wanaweza kuona changamoto zilizotatuliwa na zile ambazo bado hazijatatuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya makongamano mbalimbali ambayo tumekuwa tukitoa elimu kuhusiana na masuala Muungano, nakushukuru.

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni changamoto gani mpya za Muungano zimejitokeza?

Supplementary Question 2

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa maelezo ya Waziri kwamba hakuna changamoto mpya ni kumshukuru Mwenyezi Mungu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto za zamani bado hazijakamilika. Ikiwemo hasa changamoto ya bandari na hili suala la bandari limekuwa linaleta kelele nyingi kwa wananchi na limekuwa kero kubwa. Kwa nini Serikali haioni haja ya kulichukulia jambo hili kwa udharura wake na kulitatua haraka iwezekanavyo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge. Katika kikao chetu ambacho tulikaa mwezi wa sita tulikubaliana na tulitoa maelekezo. Kwa sababu vikao hivi huwa tunakaa na Wizara za pande zote mbili au pande zote mbili zinagusa Muungano. Tulitoa maelekezo na maelekezo haya yamekwisha anza kufanyiwa kazi kwamba, watu wa TRA na wengine wa Bandari wanaohusika waende wakakae washughulikia hili jambo, tuweze kuambizana zipi zitakuwa zinalipiwa kama sehemu ya changamoto na zipi hazilipiwi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie Mheshimiwa kwa kuwa Kamati zinaendelea kukaa, hili jambo tunakwenda kuzimaliza ili kuimarisha Muungano wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, ni changamoto gani mpya za Muungano zimejitokeza?

Supplementary Question 3

MHE. KHALIFA MOHAMMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa changamoto ambazo bado hazijatatuliwa ni upelekaji wa sukari ya Zanzibar katika soko la Tanzania Bara. Ni lini kero hii ambayo ni ya muda mrefu itatatuliwa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba moja ya miongoni mwa mambo ambayo Kamati zimo mbioni kuhakikisha kwamba tunaliweka sawa ili kuondosha hii kama ni sehemu ya changamoto ya Muungano ni hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili ni jambo ambalo kama tulivyosema hapo awali kwamba jambo hili la utatuzi wa changamoto za Muungano limetengenezewa kamati maalumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe waheshimiwa Wabunge, ikiwa tumeweza kutoka tangu changamoto ya kwanza leo tumezipata changamoto 22 maana yake na hili kupitia Kamati zinazohusika kwa mujibu wa taratibu zote linakwenda kutatuliwa ili kupunguza changamoto kubwa ambayo inakabili Muungano wetu.