Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, kwa nini Halmashauri ya Magharibi “A” imeweka Sheria ya Kodi na VAT kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishukuru Serikali kwa jibu. Pamoja na kwamba jibu hili limejibiwa kisiasa zaidi kuliko tatizo lilivyo, ningeomba Mheshimiwa Waziri atuambie ni lini sasa Serikali au Wizara itakuwa Serious Kujibu matatizo yetu ambayo yanaongozwa na Sheria? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; kwa sababu imeonekana Sheria hii inafanya kazi zaidi kwenye upande mmoja lakini kuwaathiri Wabunge wa Majimbo kwa upande wa Zanzibar. Je, Serikali sasa haioni iko haja ya kuwaandikia wenzetu wa Zanzibar ili waache kuvunja Sheria iliyotungwa na Bunge hili?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira tuko serious katika kufanya kazi zetu. Tupo serious kufanya kazi zetu kwa mujibu wa sheria na taratibu zote zilizowekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii inayafnya kazi kwa upande huu wa Mfuko wa Jimbo iko Sheria inayosimamia Mfuko wa Jimbo. Lakini ipo Sheria inaitwa Zanzibar Revenue Administrative Act. Sheria ambayo inasimamia na imetoa mamlaka kwa halmashauri na Mabaraza ya Miji kutoza ama kukata kodi kutokana na sehemu ya fedha zinazoingia kwenye halmashauri zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuko serious na kutokana na u-serious tulionao tunakwenda kutatua changamoto zote ambazo zinakabili Mfuko wa Jimbo hasa katika Jimbo la Mwera na maeneo mengine yote kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, nimwambie Mheshimiwa kwamba tuko tayari kama ushauri wake alivyosema kwamba tuandike barua lakini nataka nimfahamishe tunavyo vikao vinavyohusika na kujadili changamoto hizi na majadiliano yote yanayohusiana na Mfuko wa Jimbo. Vikao ambavyo vinaanza katika ngazi nyingi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tayari tumekwishaandaa kikao kazi ambacho tunakwenda kukaa viongozi wa halmashauri zote, viongozi wa mabaraza ya miji, Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais ili lengo na madhumuni na Wabunge wote tuweze kuelezana hizi changamoto zinazogusa Mfuko wa Jimbo hasa kwa upande wa Zanzibar.