Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itawahamisha wataalam wa maendeleo ya jamii kuwa chini ya Wizara?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini hata hivyo swali hili naona halipaswi kujibiwa na Wizara hii. lakini nitauliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa kuna baadhi ya Wizara kama vile Wizara ya Ardhi na Wizara ya Afya imeweza kuhamisha wataalam wa kada zinazoendana na Wizara zile kutoka halmashauri kwenda kwenye Wizara mama zao. Je, Serikali haioni haja sasa ya kufanya tathmini ya kina ya Sera hii ya Ugatuaji ili kuendana na mahitaji halisi ya sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu namba mbili; kwa kuwa sasa kumekuwa na wimbi kubwa la upotofu wa maadili nchini, kama vile ukatili wa watoto na wanawake. Je, Serikali haioni haja katika Ofisi ya Sekretarieti ya Mkoa (RAS) kuwepo na RAS Msaidizi kwa ajili ya maendeleo ya jamii? Kwa sababu mpaka sasa hivi ofisi zote za mkoa hakuna RAS Mmsaidizi kwa ajili ya issues za maendeleo ya jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Dr. Dorothy Onesphoro Gwajima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu langu la msingi kama nilivyosema kwamba Serikali sasa baada ya kuundwa kwa Wizara hii mpya inaendelea kuangalia utaratibu gani mzuri utaweza kuimarisha uratibu au mfumo wa ngazi ya mkoa mpaka kwenda kwenye halmashauri ili Wizara hii ambayo sasa hivi inakabiliwa na changamoto nyingi za kijamii iweze kufanya kazi kwa uharaka na ufanisi kwa kuwatumia wale wataalam wake. Hivyo basi niseme kwamba nimepokea mchango wake na tunapoendelea na majadiliano haya ya kuimarisha hii mifumo tutawasilisha ili Serikali kwa ukubwa wake na upana wake iweze kuangalia.

Lengo letu ni kuhakikisha kwamba huduma zinazotolewa kule na wataalam hawa ziko vizuri wakati wote na za haraka na jamii inabadilishwa fikra zao ili kupokea maelekezo na matakwa ya utekelezaji wa sera zingine zote. Naweza nikaweka hivi kwa ujumla wake.