Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa wodi ya mama na mtoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ambayo ujenzi wake umesimama?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapozungumzia hospitali ambazo ni kielelezo na zipo mpakani ni Hospitali ya Kyela, lakini hospitali hii ni hospitali kongwe sana ambayo kwa sasa hivi haitamaniki na hata ukifanya usafi haioneshi kwamba ni hospitali ambapo watu wanaweza wakatibiwa na kupata faraja.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kwa Serikali kuhakikisha majengo haya yanajengwa upya na yanakuwa mapya kwa ajili ya kuwa na manufaa kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; ikama ya wafanyakazi walioko katika Wilaya ya Kyela imepungua sana na iko kiwango cha chini kukidhi mahitaji ya magonjwa mengi ambayo yako Kyela.

Je, Serikali haioni haja ya kuongeza wafanyakazi kwa kipindi hiki?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mlaghila Jumbe; la kwanza la fedha kutengwa kwa jili ya ukarabati wa hospitali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kama nilivyokuwa nimeshasema kwenye majibu yangu ya msingi, tayari Serikali imeshatenga fedha zaidi ya bilioni 2.75 ambazo zimekwenda katika Hospitali ya Wilaya ya Kyela ili kuhakikiusha kwamba inafanyiwa ukarabati; na katika mwaka huu wa fedha tumetenga shilingi milioni 800 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi huo. Nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge, kwamba ni adhma ya Serikali hii ya awamu ya sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha inakarabati hospitali kongwe zote nchini, ikiwemo ya Kyela, na tutaendelea kutafuta fedha kufanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali la pili la ikama ya watumishi. Bunge lako tukufu hili ni mashahidi, Serikali imetangaza ajira zaidi ya 21,300 kwenye sekta ya elimu na sekta ya afya. Ajira hizi zitakapokamilika tutahakikisha vilevile Hospitali ya Kyela inapata wataalamu ambao wanatakiwa kuhudumia Watanzania waliopo Kyela pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.