Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Wakazi wa Kichangani katika Wilaya ya Mpanda Mjini hawajawahi kupata hati kwa ardhi wanayomiliki:- Je, ni lini wananchi wa maeneo hayo watapatiwa hati zao hasa ikizingatiwa kuwa zimechukua muda mrefu sana na haijulikani hatma yao ni nini?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Wilaya ya Mpanda Manispaa nusu ya eneo lake halina ramani kabisa hususan Semulwa, Kichangani, Makanyagio kuelekea Misunkumilo pamoja na majengo ya katikati ya mji; na kwa kuwa, Serikali inasema sasa TRA itachukua kodi kila eneo na hawa wananchi hawana hati wala uhakika wa eneo lao kwa sababu mpaka sasa hivi hakuna upimaji wa aina yoyote na Wilaya ya Mpanda ni Wilaya Kongwe, je, Serikali itapima lini maeneo hayo ili wananchi sasa watambue haki yao ili waweze kupata mikopo kutoka kwenye benki zetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Wilaya ya Mpanda Manispaa Mabwana Ardhi wanachukua mashamba ya wananchi na kugawa viwanja lakini wale wananchi hawawapi viwanja. Je, ni lini Serikali au ni lini tutaenda na Naibu Waziri akajihakikishie hali ilivyokuwa korofi ya migogoro ya ardhi ndani ya Manispaa ya Mpanda?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nianze na ufafanuzi wa swali lako. Tunapoongelea maeneo ambayo yako demarcated ni kwamba upimaji wake ulishafanyika kwa maana ya michoro kamili lakini bado haujatenga maeneo kukamilisha upimaji kujua kiwanja kipi kinaishia wapi. Kwa hiyo, ni maeneo ambayo tayari michoro na viwanja vipo lakini bado havijawekewa mipaka yake na kuweza kukamilika kama inavyostahili.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza la Mheshimiwa Lupembe ameeleza kwamba karibu nusu ya eneo katika wilaya hiyo bado halijapimwa na ametaja baadhi ya maeneo kama Changani, Kanyageni, Sukuma na majengo ya katikati ya mji na kwamba Wizara inasisitiza habari ya kuchukua kodi, je, ni lini tutapima? Katika jibu la msingi nimesema kwamba tayari kama Wizara tumeshagundua hayo na tumeona matatizo jinsi yalivyo na jinsi ambavyo watu wanakosa haki yao ya msingi ya kuweza kuwa na ule umiliki halali wa ardhi na kuwa na hati zao ambazo zingeweza kuwasaidia pia kufanya shughuli nyingine za maendeleo ikiwa pia ni pamoja na kujipatia fursa za kupata mikopo benki. Ndiyo maana tumetangaza zabuni na tukataka Halmashauri zote ambazo wana hayo maeneo ambayo upimaji wake haujakamilika kufanya upimaji ili tuweze kuwa na uhakika wa maeneo na watu waweze kumilikishwa ili tunapochukua kodi, basi tuchukue ile kodi ambayo ni halali na iko katika maeneo sahihi ambayo tayari yako katika utaratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni Halmashauri nyingi ambazo bado hazijakamilisha upimaji. Ndani ya Wizara tuna viwanja zaidi ya 240,258 ambavyo tayari upimaji wake upo lakini haujakamilika na Kanda ya Mashariki inaongoza kwa kuwa na viwanja karibu 102,000. Kwa hiyo, tunasema kwamba, ukamilishaji huu umetangaziwa zabuni ili uweze kukamilika na tuweze kumilikisha watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anasema, baadhi ya Maafisa Ardhi wanachukua mashamba na kupima viwanja halafu wenye mashamba hayo hawapewi stahiki zao kwa maana ya pengine ya kupewa viwanja. Naomba nirudie tena kulisema hili, tulilizungumza pia wakati tunahitimisha bajeti ya Wizara, tulishasema ni marufuku kuchukua mashamba ya watu pasipo kukamilisha fidia zao. Kwa sababu unapotaka kupanua mji, tunajua ni miji mingi ambayo imeiva katika kupimwa sasa kuwa miji halali lakini tunawataka sana wananchi wasiwe rahisi sana katika kutoa mashamba yao kwa sababu wanapunjwa sana na Halmashauri zote hazitakiwi kuchukua mashamba ya watu pasipo kukamilisha taratibu za ulipaji fidia katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Lupembe hakuna Afisa Ardhi yeyote anayeruhusiwa kuchukua ardhi ya mtu bila kumpa stahiki zake. Hata kama limeiva katika upimaji, basi taratibu zile za fidia zifanyike ndipo Halmashauri iweze kuchukua eneo hilo.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Wakazi wa Kichangani katika Wilaya ya Mpanda Mjini hawajawahi kupata hati kwa ardhi wanayomiliki:- Je, ni lini wananchi wa maeneo hayo watapatiwa hati zao hasa ikizingatiwa kuwa zimechukua muda mrefu sana na haijulikani hatma yao ni nini?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwanza nianze kwa kuishukuru Wizara ya Ardhi kwa kazi nzuri wanayoifanya. Kwa kuupendelea Mkoa wa Tanga, Wizara ya Ardhi ilitoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kuangalia mashamba ambayo hayaendelezwi lakini fedha ziko mikononi mwa mtu na Korogwe hawajafika na hawajafanya utafiti wowote na badala yake wanakwenda pale kwa ajili ya kumdanganya danganya tu Waziri wa Ardhi. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari twende wote mpaka Korogwe tukaangalie yale maeneo ambayo hawajapewa wananchi na yameachwa kama misitu ili atusaidie kutatua tatizo la wananchi wa Korogwe?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru Profesa Maji Marefu ambaye ni mtani wangu, amekuwa akifuatilia sana suala hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spka, ni kweli katika utoaji wa pesa kwa ajili ya kubaini mashamba ambayo pengine hayajaendelezwa ili tuweze kuyatwaa, Korogwe walipewa shilingi milioni 50 kwa ajili ya kazi hiyo. Cha kusikitisha ni kwamba, pamoja na pesa ile kupelekwa lakini kazi iliyokusudiwa ni kama haijafanyika kama tulivyotarajia. Hata Waziri alipokwenda alipewa taarifa za maeneo mengine na haya mashamba yaliyoko Korogwe taarifa ile haukutolewa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niseme kupitia Bunge lako hili, Wizara inapotoa pesa kwa nia njema ya kutaka kumaliza migogoro ya watu iliyoko katika maeneo hayo, tunaomba sana wale Maafisa wanaopokea hizo pesa wawatendee haki wananchi ambao wamekuwa na kero ya namna hiyo. Kwa hiyo, kwa suala la kutaka kwenda kujiridhisha katika hilo na kwa sababu Wizara ilishapeleka pesa, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Stephen Ngonyani kwamba tutakuwa tayari kwenda kufuatilia suala hilo ili tuweze kujua zile shilingi milioni 50 zimetumikaje ili hatua za kinidhamu ziweze kuchukuliwa ikiwa kama kulikuwa na ufujaji wa pesa.

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Wakazi wa Kichangani katika Wilaya ya Mpanda Mjini hawajawahi kupata hati kwa ardhi wanayomiliki:- Je, ni lini wananchi wa maeneo hayo watapatiwa hati zao hasa ikizingatiwa kuwa zimechukua muda mrefu sana na haijulikani hatma yao ni nini?

Supplementary Question 3

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa kuna baadhi ya maeneo ambayo wananchi wamelipia katika eneo la Kigamboni - Kibada na wamepewa hatimiliki na nina ushahidi kamili kwa sababu mimi ni mmojawapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ile ya Kigamboni - Kibada kuna eneo ambalo watu wamepewa hatimiliki na mpaka hivi sasa watu wameshindwa kujenga kutokana na wananchi fulani fulani wanasema ni maeneo yao na ukitaka kwenda kujenga wanaandamana. Je, Serikali inalijua hilo? Kama inalijua, italichukulia hatua gani suala kama hilo ili watu waliopewa hatimiliki waweze kujenga nyumba?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Faida Bakar kuhusiana na mgogoro ambao uko katika eneo la Kigamboni hasa katika eneo la Kibada kama alivyolitaja.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda tu kwanza nimhakikishie kwanza, migogoro ya Kigamboni ambayo imekuwepo kwa sasa ni kama imepungua na Mheshimiwa Mbunge wa eneo lile amekuwa akifuatilia mara kwa mara kuweza kujua watu wake hatima yake inakuwaje. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba, pamoja na kwamba kuna ule mradi ambao unasimamiwa na Wizara ambao umechukua karibu hekta 6,000 katika lile eneo lakini bado kuna maeneo mengine ambayo yana migogoro kama alivyoitaja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wizara imetoa maeneo katika eneo la Kigamboni ambapo kuna wapimaji ambao wamepima maeneo yao. Ni kweli kuna watu ambao wana hati zao na wameshindwa kuendeleza kutokana na migogoro hiyo. Kwa sababu mgogoro huu ni mkubwa, Wizara yangu itakuwa tayari kwenda kuhakiki katika maeneo yale yote ambayo watu wana hati zao lakini kila wakitaka kuendeleza kuna watu wanaandamana ili tuweze kuondoa mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kigamboni imekuwa kama ni jicho la Wizara katika kuona kwamba ule mpangilio unaokwenda kufanyika pale unafanyika kwa taratibu ambazo ni za kisheria na ambazo zitakuwa hazikuvunja haki za wamiliki wa awali katika upande huo. Kwa hiyo, namhakikishia tu kwamba suala hili tutalifanyia kazi na tutachunguza yale yote ambayo yanalalamikiwa katika utaratibu mzima wa umilikishaji wa ardhi.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Wakazi wa Kichangani katika Wilaya ya Mpanda Mjini hawajawahi kupata hati kwa ardhi wanayomiliki:- Je, ni lini wananchi wa maeneo hayo watapatiwa hati zao hasa ikizingatiwa kuwa zimechukua muda mrefu sana na haijulikani hatma yao ni nini?

Supplementary Question 4

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali. Kwa kuwa tunataka kwenda kwenye nchi ya viwanda na tunataka kuwawezesha kimtaji wafanyabiashara na wakulima, je, Wizara ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha kwamba mashamba ya wakulima hasa wa Mkoa wa Simiyu na Mikoa ya jirani yanapimwa na kupatiwa hati ili kusudi wakulima waweze kwenda kwenye mabenki na kukopa? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Stanslaus ametaka kufahamu ni lini Wizara itapima mashamba hayo na kuwamilikisha watu ili waweze kupata hati. Naomba niseme tu kwanza suala la kuanza kupima viwanja katika maeneo ni lazima Halmashauri yenyewe husika iweze kuyatambua na kuyabaini maeneo ambayo sasa yameiva kwa ajili ya upimaji kwa sababu siyo maeneo yote ambayo yanahitaji kupimwa kwa sasa. Kwa hiyo, tunachosema ni kwamba yale ambayo yameiva na yanahitaji kupimwa na ili kweli tuweze kupata maeneo ya kuweka viwanda kama tunavyosema nchi inaelekea kwenye viwanda lazima Halmashauri ilete mashamba hayo ambayo tayari yatakuwa yamepitia katika taratibu za kawaida za kubainishwa katika Kamati zao za Mipango Miji ili tuweze kujua sasa eneo hili linahitaji kupimwa kwa ajili ya matumizi ya viwanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima iende sambamba na mpango kabambe wa maeneo hayo kwa sababu hatuwezi kupima tu kwenye maeneo ambayo hayana plan ambayo imekaa katika utaratibu wa mpango wa muda mrefu wa maeneo hayo. Kama haya mashamba anayoyasema tayari yako katika mpango kabambe wa Jimbo lake, basi ni vizuri tukayajua ili Wizara iweze kuchukua hatua hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema, tumetenga pesa shilingi bilioni 8.8 kwa ajili ya kununua vifaa vya upimaji na vifaa vitakwenda kila kanda. Kwa hiyo, vitakapofika Kanda ya Ziwa ni wazi na Simiyu vitafika ili kuweza kupima mashamba haya ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja.