Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mikakati gani ya kudhibiti mifugo katika Bonde la Ihefu na Mto Kilombero?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, ili kuzifanya juhudi hizi ambazo Mheshimiwa Waziri amezieleza hapa kuwa endelevu, Je, hatuoni haja ya kuja na mkakati wa pamoja ambao utazishirikisha sekta za maliasili, kilimo, mifugo pamoja na sekta ya maji ili kulimaliza kabisa tatizo hili ambalo ni la muda mrefu?

Swali la pili, kwa kuwa kuna good practices kwa wenzetu Uganda ambao wanawashurutisha wafugaji wenye mifugo wengi kutenga maeneo ya malisho toshelezi kwa ajili ya mifugo yao. Je, Serikali haioni haja ya kuiga mfano huu mzuri ili kuweza kupambana na changamoto hii ambayo inaleta migogoro kati ya wakulima, watu wa maliasili pamoja na mifugo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza ni kwamba mkakati upo wa Wizara zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Maji, tukiungana na watu wa Wizara ya Ardhi, kuandaa mipango endelevu kwa ajili ya kusiadia wafugaji wetu ili kuondoa hii migogoro ambayo imejitokeza. Kwa hiyo, jambo hilo lipo Mheshimiwa Mbunge, na tutaendelea kuliboresha zaidi ili tuondoe hii dhana ambayo imekuwa ikijengeka kila wakati ya migogoro inayotokana na wafugaji pamoja na wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutenga maeneo, hilo tayari ni agizo ambalo Serikali ilishalitoa katika Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya wafugaji, hususan wale wenye mifugo wengi ili kuondoa hii kuhamahama kutafuta malisho pamoja na maji. Utaratibu huu kwanza utaboresha mifugo wetu wa kisasa na kuongeza ubora wa malisho na mifugo ambao tunao. Ahsante sana.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, kuna mikakati gani ya kudhibiti mifugo katika Bonde la Ihefu na Mto Kilombero?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnamo mwaka 2006 Serikali iliridhia mifugo kuhamishwa kutoka Bonde la Ihefu kupelekwa Mkoani Lindi, hivi ninavyozungumza katika Wilaya za Liwale, Kilwa na Nachingwea kuna mafuriko makubwa ya mifugo na hivyo kusababisha kuwa na uhaba wa malisho, maji pamoja na huduma nyingine za mifugo.

Je, kuna utaratibu gani ambao Serikali imeupanga kwa ajili ya kidhibiti mifugo hii? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jambo la kwanza ambalo Mheshimiwa Mbunge amelieleza hapa lina ukweli kwa sababu idadi kubwa ya mifugo sasa hivi wamekuwa wakielekea upande wa kusini, ndiyo maana moja ya mipango mikakati ambayo Wizara ya Mifugo na Uvuvi tunayo sasa hivi ni kuongeza maeneo ya malisho, tunapeleka mabwawa ili ku-control sasa ule ufugaji holela. Kwa hiyo, jambo hilo tumelipokea kwa umuhimu mkubwa na tutaleta mpango kazi kwa ajili ya maeneo hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyaainisha, ahsante sana. (Makofi)