Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, lini Serikali itarejesha utoaji ruzuku ya pembejeo za dawa kwa Wakulima wa Kahawa ili wazalishe zaidi kama awali?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa fursa. Nina maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na kwamba mmeanza kugawa miche ili tuboreshe uzalishaji wa Kahawa. Kwa kuwa mmegawa miche; je, sasa Serikali ina mikakati gani ya kuboresha zile skimu za umwagiliaji za asili ili tuweze kuongeza tija kwenye kuzalisha kahawa, kwani bila maji hata hiyo miche haitakuwa inafanya vizuri sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Je, Serikali ina mkakati gani wa kusindika kahawa aina ya Arabica kwa sababu kahawa hii ina soko zuri sana katika soko la Dunia na kuna teknolojia nyingi za kawaida tu ambazo zinaweza zikatumika tukapata chapa au brand yetu: Je, Serikali ina mkakati gani wa kutusaidia kusindika kahawa hizi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza la kuhusu skimu za umwagiliaji wa mifereji ya asili, tunao wakandarasi ambao wako katika Mkoa wa Kilimanjaro, wanaotekeleza miradi ya umwagiliaji, wameshapata maelekezo watakwenda kukarabati na kujenga mifereji yote ya asili inayogusa jimboni kwa Mheshimiwa Ndakidemi, kwa Mheshimiwa Saashisha pamoja na kwa Mheshimiwa Dkt. Kimei.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, Serikali inao mkakati wa dhati kabisa kuhakikisha kwamba tunaendelea kusindika kahawa yetu na tusiuze kahawa ambayo haijasindikwa. Hivi sasa Bodi ya Kahawa imeshatoa zaidi ya leseni 20 kwa ajili ya wasindikaji ili kuchochea usindikaji wa zao la kahawa na mwisho wa siku tutengeneze masoko ya uhakika. Hivi sasa tumepata nafasi kahawa yetu inauzwa sana na kupekekwa Japani ikiwa ni sehemu ya kazi nzuri ambayo imefanywa katika hatua ya awali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, kazi hii inaendelea.