Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GHATI Z. CHOMETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu ya maji mashuleni ili kuepusha milipuko ya magonjwa?

Supplementary Question 1

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, changamoto hii ya miundombinu ya maji mashuleni bado ni kubwa sana hasa katika Mkoa wa Mara. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha ina peleka miundombinu hii ya maji katika shule za Mkoa wa Mara?

Swali la pili, kwa kuwa sasa Serikali inatekeleza miradi ya ujenzi wa madarasa, ujenzi wa mabweni katika shule zetu. Je, haioni haja sasa ya kutenga fungu maalum wakati ikitekeleza miradi hiyo, inaweka na fungu la utekelezaji wa miundombinu hiyo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Chomete, swali la kwanza juu ya mkakati wa Serikali kuhakikisha changamoto hii inaisha.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, mradi huu wa SRWSS ni wa miaka mitano na utaisha mwaka wa fedha 2024/2025 na value yake jumla ni shilingi bilioni 119.6, hivyo basi Serikali inaendelea kadri siku zinavyokwenda kupunguza changamoto kwenye mashule kupitia mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili la miradi yote inayotekelezwa sasa ya ujenzi wa madarasa na ujenzi wa shule mpya, katika shule zinazojengwa hivi sasa, shule mpya lakini katika ukarabati wa vyumba vya madarasa kwenye shule mbalimbali nchini kupitia miradi ambayo ipo ya EP4R, SEQUIP, BOOST na LANES na mingineyo, component ya matundu ya vyoo vilevile na maeneo ya kuoshea mikono ipo, kwa hiyo sasa hivi Serikali inapopeleka fedha katika maeneo mbalimbali inahakikisha na hizi facilities zinakuwepo.