Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Tengeru utatekelezwa ili kuongezea mapato na kuboresha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika,ahsante kwa kunipa nafasi sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza, nishukuru sana kwamba Serikali ina mpango wa kutekeleza mradi wa ujenzi wa soko la kisasa eneo la Madiira, lakini ningependa kujua kwamba huo mradi utaanza lini?

Pili, soko hili la Tengeru tunalolizungumzia hapa ni soko maarufu sana la wafanyabiashara hasa akina mama wanafanya biashara zao kwa mateso makubwa wakati wa mvua, kwa sababu wanafanya kwenye matope na mvua nyingi lakini pia wakati wa jua wanaungua jua.

Je, Serikali haioni sasa ni busara kuliboresha soko hili kwa kujenga hanga kama Machinga Complex ya Dodoma? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali yake mawili Mheshimiwa Pallangyo kwanza kuhusu mradi huu utaanza lini?

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, mradi huu utaanza pale ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Meru itawasilisha michoro yake Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili na sisi tuweze kuipitia na kuona ni namna gani ambavyo tunaweza tukafanya marekebisho na baadae tukaipeleka Wizara ya Fedha kwa ajili ya kupata fedha kwenye miradi ya kimkakati kama Halmashauri nyingine zinavyopata.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili la kuboresha eneo la soko hili. Hizi zinatakiwa pia ziwe jitihada za Mkurugenzi wa Halmashauri pale ya Meru. Tumeona hapa katika mradi anaoutaja wa Jiji la Dodoma ilikuwa ni mradi wao wenyewe wa Jiji na wametumia mapato yao ya ndani kama Jiji la Dodoma, tumeona katika Halmashauri nyingine nchini kama Shinyanga ambapo wamejenga soko la machinga wadogo wadogo hawa kwa hela zao wenyewe za ndani na maeneo mengine ya Halmashauri zetu hapa Tanzania. Hivyo basi, nichukue nafasi hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru kuhakikisha anatenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa soko kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo wadogo.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Tengeru utatekelezwa ili kuongezea mapato na kuboresha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wakati Mheshimiwa Rais alipofanya ziara Arusha, wananchi wa Jimbo la Meru Magharibi katika Kata ya Kisongo Mateves alituahidi soko: -

Je, ni lini sasa Serikali kupitia TAMISEMI itajenga soko la Kisongo Mateves?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa sababu hii kama anavyosema Mheshimiwa Lembris ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, tutakaa na wenzetu wa Halmashauri ya Wilaya kuona kama michoro iko tayari iwasilishwe Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuiombea fedha Hazina na kuanza ujenzi wake mara moja.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Tengeru utatekelezwa ili kuongezea mapato na kuboresha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika,ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Rungwe soko la Kiwira ni soko maarufu kwa ndizi lakini lina mazingira magumu. Ni lini Serikali itatuongezea fedha kwa ajili ya kulijenga liwe la kisasa?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itaongeza fedha kwa ajili ya soko hili la Kiwira pale Wilayani Rungwe kadri ya upatikanaji wa fedha lakini ni wao wenyewe kupitia Mkurugenzi wa Halmashauri kuwasilisha maombi hayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuweka katika miradi ya kimkakati na kuanza ujenzi wa soko hili la Kiwira.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Tengeru utatekelezwa ili kuongezea mapato na kuboresha huduma kwa wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mji wa Chemba ni Mji ambao unakuwa kwa kasi sana lakini hauna soko, naomba kujua nini mkakati wa Serikali kujenga soko katika Mji wa Chemba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali unaanza na wao wenyewe Halmashauri ya Wilaya, hatuwezi tukakaa Ofisi ya Rais, TAMISEMI tukajua kuna uhitaji wa soko katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, ni wao kupitia Baraza lao la Madiwani liibue mradi huu na kisha kufanya andiko kupitia Mkurugenzi na Afisa Mipango wake na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya kuwajengea soko wananchi wa Chemba.