Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka utaratibu kwa wananchi kuwasilisha Hoja Binafsi mbele ya Mabaraza ya Madiwani?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Pamoja na demokrasia yetu ya uwakilishi nchi zilizoendelea wamekuwa na utaratibu wa kupokea hoja za wananchi za kimaendeleo na pale wanapoziona zina maana mwananchi huyo huitwa kuja kutetea hoja yake na ambayo inaweza kutumika kwa ajili ya kuendeleza eneo husika, jambo hili limeendelea kufanyika katika nchi nyingi zilizoendelea.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, hivi karibuni Serikali imesitisha utoaji wa asilimia kumi kwa akina mama, vijana na watu wenye ulemavu. Kwa kuwa jambo hili lina maslahi mapana ya nchi yetu. Je, Serikali haioni haja ya kuruhusu kwamba sasa wananchi watoe maoni kuhusu jambo hili, namna bora ya kuweza kulitekeleza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la Mheshimiwa Nollo ni kwamba wananchi wanapewa fursa ya kuhudhuria Mabaraza ya Madiwani na kusikiliza mijadala ambayo inaendelea, kama kuna hoja mahsusi kwa mwananchi au ana idea yoyote ambayo anataka kuiwasilisha anaweza akaonana na Mwenyekiti wa Halmashauri, akazungumza nae na kumpa wazo hilo, kisha Mwenyekiti wa Halmashauri anawasilisha lile kwa wenzake ambao ni Baraza la Madiwani, wakiona inafaa anaalikwa yule mwananchi ili aweze kutoa presentation mbele ya Baraza la Madiwani.

Mheshimiwa Spika, utaratibu huo upo, kwa hiyo niombe tu wananchi wa kule Bahi na maeneo mengine, kuhakikisha kwamba kama kuna mwananchi ana idea nzuri ya kusaidia jamii na Halmashauri, basi awasiliane na Mwenyekiti wa Halmashauri ili Mwenyekiti wa Halmashauri aweze kuongea na Madiwani wenzake na kumkaribisha mwananchi huyo katika Mabaraza ya Madiwani kwenda kufanya presentation. (Makofi)