Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mwembe – Mbaga hadi Mamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii ni mara ya tatu kama siyo ya nne tunauliza swali hili tunaambiwa kwamba Serikali itatafuta fedha. Tunaomba kauli ya Serikali, ni lini fedha itapatikana? Hii ni ahadi ya Rais toka mwaka 2005 mpaka leo fedha za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina hazijapatikana? Hilo la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Kata ya Mhezi, Mshewa na Msindo, barabara hii inaponyesha mvua kidogo inaharibika sana kiasi ambacho magari hayapiti kabisa. Kwa hiyo, mawasiliano yanafungwa kati ya Kata hizo na Same: Je, ni lini Serikali itaweka zege katika barabara hiyo kwa maeneo hayo niliyoyataja kabla ya upembuzi yakinifu na upembuzi wa kina kukamilika ili barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi, tunatambua umuhimu wa barabara hii na ndiyo maana katika jibu la msingi nimesema tunaendela kutafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri barabara hii mimi nimetembelea yote na tulishatoa maagizo na tayari tumeshaainisha maeneo yote korofi likiwemo eneo hilo la Msindo, Mshewa na Mhenzi. Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kilimanjaro ameshatengeneza bajeti na hivi ninavyoongea amesha-submit kwa Mtendaji Mkuu wa TANRIOAD ili aweze kutoa fedha kujenga hayo maeneo korofi ama kwa lami nyepesi ama kwa zege ili barabara hii iweze kupitika yote kwa mwaka mzima, ahsante.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mwembe – Mbaga hadi Mamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya Msongola – Mbande nilipewa ahadi kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023 itakamilishwa yote kilometa 4.95 kwa kiwango cha lami. Naomba commitment ya Serikali kutimiza ahadi hii iliyotolewa mwaka 2022 hapa Bungeni? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara aliyoitaja ambayo inaanzia Pugu – Mvuti – Msongola – Mbande inaunganisha majimbo mawili; Jimbo la Mheshimiwa Silaa na Jimbo la Mbagala la Mheshimiwa Chaurembo. Tuna kilometa nne point ambazo bado hazijakamilika. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti tunayokwenda kuitekeleza tutakamilisha kwa lami kipande kilichobaki, ahsante. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mwembe – Mbaga hadi Mamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara inayotoka Kahama – Busangi – Chela – Nyang’wale mpaka Busisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja tunakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa maana ya kutoka Kahama kwenda Busisi. Pia, baada ya hapo ndiyo tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mwembe – Mbaga hadi Mamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Galapo, Orkasmet hadi Kibaya Kiteto? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, tunapoongea sasa hivi, barabara aliyoitaja ndiyo tunakamilisha usanifu wa kina na baada ya hapo tutatafuta fedha kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.