Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga angalau kilometa tano kwa kiwango cha lami Barabara ya Tunduru - Mtwara Pachani?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mwili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Je, ni lini ujenzi huo wa mita 500 utaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Barabara hii ya lami inapita katikati ya Mji na ndiyo kwenye sura ya Wilaya ya Tunduru: Je, ni lini Serikali itatufungia taa za barabara ili kusaidia ulinzi na usalama nyakati za usiku? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mita 500, tunavyoongea mkandarasi ameshapatikana na sasa hivi anajiandaa, yuko kwenye mobilization kuanza kujenga hizo mita 500 kwa mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, habari njema kwamba mwaka ujao katika huo mji ambao taasisi zote zinapita katika barabara ya TANROADS, tutajenga kilometa 2.1 na kuweka taa eneo lote katika mji huo wa Tunduru, ahsante. (Makofi)

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga angalau kilometa tano kwa kiwango cha lami Barabara ya Tunduru - Mtwara Pachani?

Supplementary Question 2

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika barabara ya Tunduru – Nalasi, kipande cha kutoka Chiwana mpaka Mbesa kina matatizo ya kupitika wakati wa mvua: Je, ni lini Serikali itaweka lami nyepesi kwenye kipande hicho wakati wanasubiri fedha za kujenga kipande hicho?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi na barabara hii niliitembelea, Waziri alishaahidi na mimi nilipita. Maeneo yote korofi tumeyaainisha na tumetoa maelekezo kwa Meneja wa Mkoa wa Ruvuma kwamba barabara hii yenye urefu wa kilometa 300 maeneo yote ayafanyie kazi kwa maana ya kuainisha maeneo korofi na pia kujenga kwa kiwango cha zege ama lami maeneo yote korofi ili barabara hii iweze kupitika kwa mwaka mzima, ikiwa ni pamoja na eneo alilolitaja Mheshimiwa Mbunge, ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. HASSAN Z. KUNGU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga angalau kilometa tano kwa kiwango cha lami Barabara ya Tunduru - Mtwara Pachani?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, barabara ya njia nane kilometa 19.2 kutoka Kimara hadi Kibaha, imekosa kabisa vituo vya dala dala kwa abiria kupumzika; kwa hiyo, wanaumia na jua na mvua: Je, ni lini Serikali itatengeneza hivi vituo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Japo suala hili Mheshimiwa Mbunge amekuwa akilileta mara kwa mara, lakini nimhakikishie kwamba pia Kamati ya Miundombinu imeshatoa maelekezo kwa Wizara kuhakikisha kwamba suala hili inalifanyiwa kazi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili tumeshaliona na tayari Wizara imeshalipokea kwa ajili ya kutengeneza hivyo vituo kama alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge, ahsante sana.