Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kutoa mwongozo kwa wawekezaji kuchangia shughuli za maendeleo katika maeneo wanayowekeza?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa Jimboni Kibaha Vijijini kuna kongani kubwa ya viwanda Kwara na viongozi wa eneo hilo hawana uelewa wa kutosha juu ya miongozo hiyo. Je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kufika Jimboni Kibaha kuwapa mwongozo ili waweze kusimamia chanzo hiki cha mapato?

Swali la pili, kwa kuwa maeneo ya Kibaha Vijijini , viwanda vingi vitajengwa na vingine vitatumia Sheria ya EPZ. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kubadilisha sheria ili viwanda hivi vitakavyojengwa kwenye EPZ viweze kuchangia shughuli ya maendeleo? (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli Kibaha katika Mkoa wa Pwani ni moja ya maeneo ambayo kuna uwekezaji mkubwa sana wa viwanda hapa nchini. Kwa takwimu tulizonazo kwa Aprili tu takribani miradi saba imewekezwa katika eneo hili ambalo ni muhimu sana kwa wawekezaji wengi.

Mheshimiwa Spika, Wizara na Serikali kama nilivyosema, maeneo yote ya uwekezaji pamoja na eneo la Kwala Industrial Park ambalo linajengwa pale, tunawaelekeza wawekezaji kuhakikisha wanachangia maendeleo na miradi ya kijamii. Pili katika maeneo hayo tumeshaweka kwenye Serikali za Mitaa Idara Maalum ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara ambao kazi yao wao ni kuwaelimisha wawekezaji hawa kwa kushirikiana na TAMISEMI kuhakikisha wanachangia mapato wanayopata kutoka na uwekezaji huo.

Mheshimiwa Spika, pili, kwenye maeneo ya uzalishaji kwa ajili ya mauzo nje EPZ tumeshasema na tunao mpango wa kuweka utaratibu wa uwekezaji, ambao unaelekeza wawekezaji hawa ambao wanafaidika, wananufaika na vivutio maalum ambayo kimsingi ni kodi za Watanzania, kuhakikisha mapato wanaopata au faida wanazopata kutokana na uwekezaji huo waweze kurudisha kwa wananchi kupitia shughuli mbalimbali za kijamii, kama ni elimu, afya, maji au barabara kulingana na mahitaji ya maeneo husika ambayo wanawekeza wawekezaji hao, nakushukuru sana.