Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, mbegu za kisasa tunazozitumia unaweza kuzitumia mara moja tu na ni bei ghali. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuendeleza mbegu zetu za asili ambazo unaweza kuzitumia zaidi ya mara moja ili kupunguza gharama kwa wakulima?

Swali la pili, mwaka 2020 Wizara ya Kilimo ilikuja Jimboni Hanang’ na baadaye wakanunua ngano, tukielezwa kwamba zile ngano zilizoko Hanang’ ni bora na zinafaa kuwa mbegu. Je, Serikali ina kauli gani juu ya upatikanaji wa mbegu bora za ngano Nchini? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la kwanza mbegu za asili, mbegu hizi zimeendelea kutambuliwa na Taasisi ya Utafiti ya Kilimo Tanzania (TARI) inaendelea kuzifanyia utafiti, vilevile Mamlaka ya Afya, Mimea na Viuatilifu Nchini (TPHPA) na yenyewe sasa iko mbioni kwa ajili ya kutunga Sheria ya Nasaba za Mimea ili kuzitambua, kuzitunza na kuzitumia kwenye utafiti. Kwa hiyo, Serikali inaipa umuhimu suala hili la mbegu za asili.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kweli mwaka 2020 tulifanya utafiti huo na tulichukua sampuli ya mbegu 22, tano zikiwa kutoka nje ya nchi na 17 za ndani ya nchi, kwa ajili ya kwenda kuangalia ubora wake. Katika tafiti hii zaidi ya mbegu 10 zimeonekana zinafanya vizuri na zina kiwango kikubwa cha gluten kwa maana ya protein ambayo inazidi asilimia 10, hivi sasa zimeanza kusambazwa katika baadhi ya maeneo kuweza kutumika ili kusaidia upatikanaji wa mbegu bora za ngano.

Mheshimiwa Spika, katika mbegu hizi ziko mbegu za Kariege, Sasambua, Sifa, Chiriku pamoja na mbegu nyingine ya Mbayuwayu ambayo imeonekana kuwa na soko kubwa sana.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Je, Wizara ya Kilimo inaonaje ikitumia muda huu kufungua dirisha la kuwakopesha wakulima mbegu, mbolea, viuatilifu na vitendea kazi vingine ili kujiandaa na msimu wa kilimo ambao unakuja? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hivi sasa Wizara ya Kilimo kupitia Wakala wa Mbegu tupo katika utaratibu wa kuanza kusambaza mbegu kwa msimu unaokuja, kwa kufungua madirisha kupitia hayo maeneo tofauti tofauti. Vilevile tunao Mfuko wetu wa pembejeo ambao nao ni mahsusi kwa ajili ya kuwasaidia wakulima kuweza kupata pembejeo hizi kwa wakati na kwa bei nafuu. Hivyo nitumie fursa hii kuwaomba wakulima wote nchini Tanzania kutumia madirisha haya mawili kwa ajili ya kuweza kupata pembejeo hizi kwa wakati ili wakati wa msimu wawe tayari wanazo na kuanza kutumia kwa ajili ya kilimo.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 3

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba ni kwa nini Serikali wanaendelea kufanya utafiti wa mbegu za asili ambazo zimetukuza wote mpaka hapa tulipo badala ya kuzalisha kwa wingi na kuzisambaza? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika majibu yangu nimezungumza kwamba tayari Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu pale Arusha wanayo benki na wanaendelea kuzitunza mbegu hizi kwa ajili ya usambazi. Kwa hiyo, zoezi la usambazi na kwenye kilimo utafiti haukomi vitakwenda sambamba lakini mwisho wa siku ni kuhakikisha kwamba mbegu hizi zinawafikiwa wakulima kwa wakati. Kwa hiyo, mamlaka inafanya kazi hiyo vilevile utafiti hauwezi kukoma kwa sababu ni kila siku mambo mapya yanajitokeza.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA K.n.y. MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka mbegu za mahindi kabla ya kipindi cha masika katika Jimbo la Mbulu Vijijini?

Supplementary Question 4

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo iliahidi kupeleka mbegu bora za soya kwenye vijiji vingi vilivyopo Jimbo la Ndanda ikiwemo Kijiji cha Mumburu kwa sababu soya ilikuwa inalimwa hapo zamani, ni mwaka wa tatu sasa mbegu hiyo haijaenda.

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kupeleka mbegu kwenye maeneo hayo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nimesikiliza hoja ya Mheshimiwa Mbunge, nimeichukua. Tutakwenda kuifanyia kazi ili wakulima wake waweze kupata mbegu za soya. (Makofi)