Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Kwa kuwa kumekuwa na malalamiko mengi sana kuhusiana na kikokotoo hicho na inaelekea hakuna mpango wa kukirekebisha.

Je, Serikali imejipangaje hata hicho kiasi ambacho kinatolewa, kitolewe kwa wakati?

Swali la pili, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wastaafu sasa hasa wale wanaopata kiasi cha chini, mathalani shilingi 100,000 kwa mwezi, wanaongezewa kiwango hicho cha chini cha pensheni kwa kadri ambavyo mishahara inavyoongezeka?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Priscus Tarimo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosisitiza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba, ndiyo maana tunaendelea kutoa elimu. Suala la kwamba kuna malalamiko, wanufaika wa mifuko hii ya pensheni, katika utoaji wa fedha kulikuwa kuna changamoto ya uwiano wa utoaji wa mafao, pia kulikuwa na changamoto ya uendelevu wa mifuko, tulikuwa na changamoto pia ya mkupuo wa malipo, kwa sasa katika mkupuo wa malipo wanufaika ni asilimia 81 ya wanachama wote, asilimia 19 mafao yao ya kila mwezi yameongezeka.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa katika mkupuo wa malipo, wanufaika ni asilimia 81 ya wanachama wote, na asilimia 19% mafao yao ya kila mwezi yameongezeka. Pia katika kipindi hicho utaweza kuona kwamba katika malipo yale ya kila mwezi, ilikuwa wanaweza kulipwa kwa asilimia 50, lakini sasa yamefikia asilimia 67 ya malipo. Hayo ni maboresho ambayo yametokana na utafiti uliofanyika. Tulifanya actuarial valuation, kwa kuwa mifuko hii ilikuwa na hali mbaya.

Mheshimiwa Spika, utakumbuka tulikuwa tuna mifuko mingi ya GPF, PSPF, LAPF na NSSF. Mifuko hii kwa ujumla ilikuwa inashindana kwa wanachama wale wale. Utaratibu na maamuzi ya kuiweka pamoja mifuko hii imeleta tija kubwa na sasa mifuko imetoka from loss making trend to profit making venture. Kwa sehemu kubwa utaweza kuona, katika utaratibu huu, ndiyo maana tunaendelea kutoa elimu kwa sababu faida ni nyingi kuliko hasara ambazo zilikuwepo hapo awali.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli tutaendelea kutoa elimu. Mheshimiwa Mbunge kama anadhani kuna watu wanalalamika, wote ambao wamekuwa wakifika kwa kutokuelewa utaratibu huu ofisini, wamekuwa wakipewa elimu na wameona faida hii. Namwomba Mheshimiwa Mbunge, kama anao watu hao, nitashirikiana naye katika kutoa elimu kama jinsi ambavyo mifuko imeendelea kutoa, ahsante.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wako watumishi wa Serikali wakiwemo walimu ambao walikumbwa na mfumo huo wa kikokotoo wa muda katika kile kipindi ambacho kilianza kutumika, lakini mpaka sasa walimu hao mfumo wao wa pensheni haueleweki na hauko sawa: Nini kauli ya Serikali kuhusiana na walimu hao? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama alivyouliza kwamba mifumo ya ulipaji wa mafao ya walimu haueleweki.

Mheshimiwa Spika, huu utaratibu uliofanyika wa kuunganisha mifuko na kutengeneza uwiano sawa wa malipo haukuacha kundi lolote nje likiwemo kundi la walimu. Kwa hiyo, kama kuna sehemu ambayo anadhani kwamba kuna walimu wana changamoto hiyo, mimi nilipokee tu jambo hili kutoka kwake na nikalifanyie kazi, kwa sababu mfuko huu haujabagua kundi lolote katika kutengeneza maslahi ya wafanyakazi wetu, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika jibu ambalo Mheshimiwa Waziri ametoa, amesema wanufaika kwa sasa hivi wameongezewa pesa kwenye yale mafao ya kila mwezi, lakini lalamiko lao kubwa ni mafao ya mkupuo ambayo mmetoa asilimia 50 mpaka 30. Leo mtu anayestaafu ambaye angepaswa kulipwa shilingi milioni 100, anapata milioni 50. Huo ndiyo msingi wa swali: Ni lini mtaleta sheria mbadilishe ili wastaafu wapate asilimia 50 waweze kujikimu ili sasa wakipata hicho cha mwezi, tayari msingi utakuwa una maana? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Nazidi kusisitiza kwamba suala hili ni la uelewa tu na elimu ambayo tutaendelea kuitoa. Mafao katika hatua ya awali katika Mifuko hii ya GEPF, PSPF, LAPF pamoja na PPF na NSSF, kila mfuko ulikuwa na aina yake ya utoaji wa mafao kulingana mfuko. Pia kwa hatua ya sasa, ukiangalia kwenye hili suala analosema la malipo ya Mkupuo, yalikuwa asilimia 25 na kwa mapenzi ya dhati Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kupitia vikao, mashirikisho ya vyama vya wafanyakazi sasa

hivi imefikia asilimia 33 ya ulipaji wa mafao hayo, hayakufika kwenye hiyo asilimia 50 ambayo anaisema kwenye hatua ya awali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, jambo hili tutaendelea kutoa elimu bila kuchoka, na wanufaika ambao ni wanachama wenyewe hawajawa na tatizo kubwa hili. Kama wapo, nazidi kusisitiza kwamba Serikali tuko tayari kuwasikiliza na kuwahudumia ili kuweza kuhakikisha manufaa hayo wanayapata. Serikali hii inawapenda sana wastaafu na ndiyo maana maboresho yamefanyika kila wakati; kisera, kisheria, kimiundo, kimfumo na utoaji. Hata kwenye utoaji sasa tumeenda katika teknolojia ya tehama, ahsante. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kikokotoo ni kwa ajili ya watumishi na wastaafu; na uhalisia ni kwamba watumishi na wastaafu hawakitaki kikokotoo hiki: Ni lini Serikali italeta Muswada hapa wa kufuta kikokotoo hiki ili kuondoa kero kwa watumishi na wastaafu ambao hawakitaki? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, no research no right to speak. Katika uhalisia wa actuarial report na utafiti uliofanyika, unufaikaji wa wanachama ni asilimia 81 ya wanachama wote, na asilimia 19, nadhani kama mtu atakuwa na hoja na hakubaliani, naye afanye utafiti na atuambie. Sisi tutaendelea kutoa elimu. Kwa kufanya hivyo, kwa sababu inaonekana suala linaanzia pengine kutokuwa na picha ya pamoja, tutaona umuhimu wa kuweka semina kwa ajili ya Wabunge ili kuweza kupata uelewa wa pamoja na kuwasaidia vizuri wanachama wetu kuliko kuwapotosha, ahsante.

Name

Mariam Madalu Nyoka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 5

MHE. MARIAM M. NYOKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, Serikali inatoa kauli gani kwa watumishi waliolipwa mafao pungufu hasa walimu; na wanapofuatilia wanaambiwa walipe gharama kwa ajili ya ufuatiliaji Dodoma? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Nyoka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa wastaafu ambao michango yao haikupelekwa, kwanza ni kosa kisheria, kwa sababu sheria zetu zinamtaka mwajiri kuwasilisha michango ya mwanachama kila mwezi, lakini pia kama kuna changamoto za hao wastaafu ambao wanaambiwa tena pia waanze kupeleka michango yao wenyewe, hilo naomba nilichukue na ni jambo serious nahitaji nilifanyie kazi siku ya leo, nikitoka hapa niongee na Mheshimiwa Mbunge kwa ajili ya hatua zaidi.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, nini mpango wa Serikali kuhusu malalamiko ya wastaafu juu ya kikokotoo kinachotumika kupiga mahesabu na kulipa mafao?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, napenda kuuliza: Ni lini Serikali itamaliza kabisa malalamiko ya wastaafu wa zamani wakiwemo wale wa Jumuiya ya Afrika Mashariki?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Masuala yote ya wastaafu tumeendelea sana kuboresha katika kuwasikiliza na pia kutatua changamoto zao. Hili suala la wastaafu wa Afrika Mashariki lilikuwa ni suala la kimahakama na Mheshimiwa kama unavyofahamu maamuzi ya Mahakama ndiyo huzingatiwa. Kwa hiyo, tutaangalia, wapo wengine ambao walikuwa kwenye hatua ya kufanya execution of decree ambayo ilitolewa na Mahakama na kulikuwa kuna hatua mbalimbali za kwenda kudai mafao hayo kwa waajiri. Kwa hiyo, liko katika utaratibu wa usukumwaji na ufuatiliaji kwa mfumo wa kimahakama, lakini kwa yale ambayo yamekuja upande wetu, tutaendelea kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, nawaomba Waheshimiwa Wabunge, kama kuna issue substantial na specific kwa wastaafu kwenye eneo na jimbo lako, nitapenda nizipate ili tuzifanyie kazi. Kwa wote waliowahi kuleta, tumezifanyia kazi. Kwa hiyo, nawaomba sana, badala ya kusubiri, basi tutumie fursa hii kuweza kufanya hiyo kazi na kwenye semina ambayo tutaitoa tena kwa mara ya pili, itatusaidia sana kuweza kupata picha ya pamoja na kutatua changamoto hizi, ahsante.