Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini ujenzi wa majengo yaliyobaki ya Kituo cha Afya Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa haya majengo yanayoelezwa yamejengwa kwa nguvu za wananchi na fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri: Ni lini Serikali kwa maana ya Wizara ya TAMISEMI itapeleka fedha kukamilisha majengo haya yaliyobaki; jengo la maabara, jengo la mochwari na jengo la mganga? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, kwanza nipongeze jitihada za wananchi wa Mlimba kwa kuweza kujenga kituo hiki cha afya kwa shilingi milioni 500. Serikali kwa sasa itatafuta fedha kadiri ya bajeti itakavyoruhusu ili tuweze kwenda kujenga maabara, mochwari na nyumba ya mganga. Tayari Mheshimiwa Mbunge hili alikuwa amekuja kulifuatilia na tunaona uwezekano wa upatikanaji wa hizi fedha katika bajeti ya mwaka huu tunaoenda kuanza 2023/2024. Kama ikikosekana hapo, basi tutenge katika mwaka 2024/2025.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini ujenzi wa majengo yaliyobaki ya Kituo cha Afya Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Ngongowele kilipata fedha za Matokeo Makubwa Sasa, tulipata shilingi milioni 250, mradi ambao umeshaisha; je, Serikali haioni imefika wakati kutupatia shilingi milioni 250 nyingine kumalizia kituo kile?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kituo hiki cha afya cha Ngongowele kule katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, Serikali itatenga fedha ya kumalizia kadiri ya upatikanaji wa fedha hizi na bajeti itakavyoruhusu.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza:- Je, lini ujenzi wa majengo yaliyobaki ya Kituo cha Afya Mlimba utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. SYLIVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Tangu mwaka 2010 tuliahidiwa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Nyarubanda, lakini zaidi ya miaka 12 mpaka leo ujenzi haujaanza: Nataka kujua, ni lini hasa ujenzi huo utaanza?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi huu katika Kata ya Nyapanda utaanza kadiri ya upatikanaji wa fedha. Tutaangalia katika bajeti hii ambayo inakuja ya 2023/2024 kama haijatengewa, basi tutaangalia kutenga fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.