Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANATONA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini maana yangu hasa ilikuwa mgawanyo wa fedha za TARURA kwa kuzingatia mtandao wa barabara katika Halmashauri zetu. Kwa mfano, ukichukua Mbeya peke yake, Rungwe ni ya pili. Mbeya Vijiji ya kwanza, mtandao mkubwa kama kilometa 1,000 na Rungwe inafuata, lakini bajeti tunayopata ni ndogo kuliko Halmashauri nyingine. Kwa hiyo, naomba Serikali ituambie ni vigezo gani vinatumika kugawanya hizi pesa za barabara katika Halmashauri zetu, kwa mfano, utakuta Halmashauri ina kilometa nyingi zaidi, lakini inapata fedha chache?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mwaka jana 2022 Mheshimiwa Rais alitembelea Rungwe akaahidi kutoa kilometa mbili za lami pale Mji wa Tukuyu: Je, ni lini fedha hizo zitakuja ili mradi huo wa barabara ya kilometa mbili za lami uweze kutekelezwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantona, la kwanza hili la vigezo vya mgawanyo. TARURA ilipokea vigezo vilevile vilivyokuwepo awali kabla ya taasisi hii kuanzishwa ambapo vilikuwa vimetengenezwa na Road Fund nchini kuweza kuwapelekea fedha Halmashauri mbalimbali. Baada ya TARURA kuanzishwa, changamoto hii Serikali imeiona na tayari Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mheshimiwa Angellah Kairuki alielekeza TARURA kufanya tathmini na kuona ni namna gani fedha inaweza ikapelekwa kulingana na barabara ambazo zipo na ukubwa wa maeneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba tayari kazi hiyo ilikuwa imeshafanyika na baada ya kazi hiyo kufanyika, sasa kuna independent team ambayo imepewa ku-verify tu, kuona. Vigezo ambavyo vitatumika sasa, ni kuona urefu wa barabara, kuangalia ukubwa wa eneo husika, vilevile kuangalia milima, wingi wa mvua, agri-connect katika maeneo hayo shughuli za kilimo zinafanyika kiasi gani, na kadhalika kuweza kutoa fedha ya kwenda kwenye barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la pili la nyongeza la kilomita mbili ambazo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan hii tutaendana kadiri ya upatikanaji wa fedha kuweza kukamilisha ahadi hii. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi za Dkt. Samia Suluhu Hassan huwa zinatekelezeka kwa wakati, na tayari tutaangalia katika bajeti ya mwaka huu kupitia Taasisi ya TARURA kuona ni nini kinaweza kikatengwa ili ahadi hii ianze kutekelezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu aliyoyatoa, naomba kuuliza swali kwamba, Jimbo la Njombe Mjini ambalo ndiyo Halmashauri kubwa kuliko Halmashauri zote katika nchi hii; je, litaangaliwa kwa namna ya kipekee katika hiyo tathmini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Njombe Mjini na maeneo mengine yote ya nchi yetu ya Tanzania ambayo Waheshimiwa Wabunge mnatokea, yataangaliwa kwa vigezo vile vile ambavyo nimevitaja hapa. Ukubwa au urefu wa barabara katika wilaya husika, kuangalia ukubwa wa eneo husika, kuangalia milima, kuangalia wingi wa mvua, kuangalia shughuli za kiuchumi kama kilimo…

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa ameshakuelewa.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Napenda kuuliza, hivi ni lini Serikali itaamua kutengeneza mikataba ya Kiswahili katika utengenezaji wa barabara?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, hili la Mheshimiwa Getere, niseme tunalichukua na tutaangalia ni namna gani tunaweza tukaboresha na kuwa na mikataba ya Kiswahili.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii nami niulize swali la nyongeza. Pamoja na kwamba Mji wa Tabora unaitwa Toronto kwa sababu ya ubora wake, lakini kuna kata nyingi ambazo zina shida pale mjini kwenye barabara, hasa Kata ya Ng’ambo, Kata ya Isevya, Kata ya Kitete, na kata nyingine; je, Serikali lini ita…

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Barabara kadri upatikanaji wa fedha hizo katika Kata za N’gambo, Isevya na Kitete katika Manispaa ya Tabora Mjini.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha Bajeti ya TARURA inazingatia mitandao ya Barabara katika Halmashauri?

Supplementary Question 5

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mbunge wangu wa Jimbo la Rungwe ameuliza swali la msingi tukizingatia Wilaya ya Rungwe ina mvua nyingi na ina mtandao mkubwa sana. Ninaomba kuhakikishiwa kwa sababu yeye ndiye swali lake Mbunge wangu ameuliza ni lini mtatutengenezea hizo Barabara za TARURA na kutupatia fedha za kutosha? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokuwa nimeishasema kwenye majibu yangu ya msingi ukiangalia mwaka wa fedha 2020/2021 TARURA katika Halmashauri ya Wilaya Rungwe ilikuwa imetengewa milioni 962 tu lakini mwaka huu wa fedha tunaoenda kuutekeleza TARURA inatengewa fedha kiasi cha shilingi bilioni 2.31 katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tunakwenda kutekeleza barabara nyingi zaidi kuliko hapo awali na hiyo ndiyo azma ya Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan.