Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga stendi za mabasi katika Halmashauri za Mkoa wa Tanga?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Miradi hiyo iliyotajwa hapo ni kwa ajili ya uboreshaji wa stendi za majiji na manispaa na kwa kuwa halmashauri ninazoziongelea haziangukii kwenye majiji wala manispaa. Je, Serikali inampango gani wa makusudi sasa kuhakikisha wanakwenda kuboresha stendi kwenye Halmashauri zetu za Wilaya ya Mkinga, Pangani, Muheza, Lushoto pamoja na Kilindi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa maeneo ya stendi pia ni moja ya chanzo cha uzalishaji wa ajira hasa kwa kina mama na vijana. Je, Serikali sasa ina mkakati gani wa kuhakikisha miundombinu ya stendi inakuwa rafiki kwa wajasiliamali? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge wa viti maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja ni kweli hazipo kwenye category ya majiji na manispaa na halmashauri hizi kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, kwamba tutaendelea kutenga fedha kupitia mapato ya ndani lakini pia kupitia Serikali kuu kwa awamu kuhakikisha kwamba stendi hizo zinajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwamba halmashauri hizo pia zipo kwenye mpango, tutaendelea kujenga kwa awamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili kuhusiana na miundombinu inayowezesha wafanya biashara. Serikali imekuwa ikijenga stendi, inajenga maeneo kwa ajili ya mama lishe na baba lishe, inajenga maeneo ambayo yanaweza ku–accomodate Machinga na wafanyabiashara wadogowadogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo suala hili litaendelea kutekelezwa, ahsante. (Makofi)