Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kuondoa sharti la kukopa kwa vikundi mikopo inayotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali ya nyongeza. Kwa kuwa changamoto ya mikopo ya vikundi imekuwa kubwa sana katika maeneo ya Jiji la Dar es salaam na hususani katika Jimbo la Kinondoni, kutokana na masharti mbalimbali wanayopewa wakopaji wanashindwa kukopa. Je, Serikali haioni haja katika hiyo mikakati yake sasa kuangalia sehemu ya mtu kukopa mmoja mmoja?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa wakinamama wengi wajasiliamali wa mitaani wanashindwa kuungana kwenye vikundi na wanahitaji kupata mikopo mmoja mmoja mwenye kuuza mandazi, vitumbua na nini. Je, Serikali imejipanga vipi sasa katika hiyo mikakati yake kuhakikisha kwamba, sasa wanaruhusiwa kukopa mtu mmoja mmoja ili aendeleze biashara yake? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Kisangi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ifahamike kwamba vikundi katika mikopo ya asilimia 10 vinatumika kama dhamana, kwa sababu wajasiliamali wanaokopeshwa kwa mikopo ya asilimia 10 ni wale ambao hawana uwezo wa kutosha kuwa na dhamana ya kupewa mkopo. Kwa hiyo, concept ilikuwa kwamba kikundi ni dhamana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tumechukua hoja hii na chini ya Mheshimiwa Waziri wetu wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutaifanyia tathimini kwenye tathimini inayoendelea nakuona uwezekano wakuiboresha kama itakuwa inatija, ahsante. (Makofi)

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: - Je, Serikali haioni sasa ni wakati wa kuondoa sharti la kukopa kwa vikundi mikopo inayotolewa na Halmashauri?

Supplementary Question 2

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Vijana wengi wa Dar es salaam wanaendesha bodaboda za mikataba. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka kushirikiana na ma-bank yanayotoa mikopo ya bodaboda bank ya NMB na bank ya CRDB ili wanapofungua sasa dirisha la mikopo hii ya asilimia 4:4:2 za vijana, wanawake waweze kutoa mikopo ya vijana kuwakwamua kwenye unyonyaji wa mikataba hii ya bodaboda? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jerry Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema utaratibu wa ukopeshaji wa asilimia 10 unafanyiwa kazi na utaboreshwa, kwa hivyo tutaona pia uwezekano wakuchukua wazo hili na kuliboresha kuona namna ambavyo utawezesha vijana kupata mikopo kwa urahisi zaidi kwa kadri ambavyo itaonekana inawezekana, ahsante.