Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Choma - Ziba – Nkinga - Simbo - Puge utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na majibu mazuri ya Waziri barabara hii ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025 na huenda pia kwenye Bajeti iliyopita Waziri aliliahidi Bunge hili kuwa atatenga fedha kwenda kuanza usanifu katika barabara hii;

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili wananchi hao waanze kufanyiwa usanifu ili barabara yao ijengwe?

Mheshimwa Naibu Spika, swali langu la pili, barabara ya Chaya – Nyaua, Chanya – Manyoni – Tabora yenye kilomita zaidi ya 200, sasa kumekuwa na msongamano wa magari mengi. Tuliomba pendekezo la kuiweka bypass ya Kigwa – Magili;

Je, ni lini Serikali itaanza usanifu wa kuiweka barabara ya Kigwa- Magili ili iweze kupata kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika kama nilivyosema, barabara hii ya Chimo – Simbo hadi Puge ilikuwa haijafanyiwa usanifu; na tayari tumeshaanza kufanya usanifu. Wakati wa Bajeti ni kweli Waziri aliahidi kwamba tutaanza kujenga kilomita 10 kwa kiwango cha lami, lakini kilomita hizi zitaanza kujengwa pale tu ambapo usanifu utakuwa umekamilika, hizo kilomita za awali kilomita 10. Barabara ya pili Serikali inaendelea kutafuta fedha ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kama alivyoomba Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Choma - Ziba – Nkinga - Simbo - Puge utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza swali Mheshimiwa Naibu Waziri. Barabara ya Kenyatta itokayo Mwanza Mjini kwenda Shinyanga ambayo tayari imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na umeshakamilika, pia usanifu umekamilika. Barabara imezidi kuwa na msongamano mkubwa;

Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha barabara hii inapanuliwa kwa njia nne? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE), Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli moja ya barabara katika majiji ambayo sasa hivi ina magari mengi ni hiyo Barabara ya Kenyatta kwenda Usagara kuelekea Shinyanga. Serikali imeshafanya usanifu na sasa hivi inatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga barabara hiyo kwa njia nne ili kupunguza changamoto kubwa ya foleni katika Jiji la Mwanza, ahsante. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Choma - Ziba – Nkinga - Simbo - Puge utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kaoze- Chombe kwenda Igonda iliyopo Sumbawanga Vijijini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE.ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii bado hatujaiingiza kwenye mpango wa kuijenga kwa mwaka huu. Lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla ya kuanza kuijenga tutatafuta fedha kwa ajili ya kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika bajeti inayokuja, siyo kwa bajeti hii; kwamba hatukuipangia fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. SEIF K. S. GULAMALI aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Choma - Ziba – Nkinga - Simbo - Puge utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ni lini mkandarasi wa kujenga Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Kilolo ataweka saini mkataba na kuanza ujenzi? Kwa sababu limekuwa ni jambo la muda mrefu na wananchi wanasubiri kwa hamu. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii kwanza inafadhiliwa na World Bank, na fedha zipo. Kinachoendelea sasa hivi ni kukamilisha tu taratibu kati ya Serikali na mkandarasi ambaye tayari alishapatikana ili aweze kukabidhiwa hiyo site kujenga hizo kilomita 33 za Iringa kwenda Kilolo.