Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, lini Serikali itarekebisha Sheria za Utumishi zilizopitwa na wakati hasa kipindi hiki cha teknolojia?

Supplementary Question 1

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na niwapongeze kwa juhudi mnazofanya za TEHAMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona sasa hivi kuna utaratibu wa viongozi wa aina moja au Maofisa wa aina moja kufungua group na kutumiana document za kiserikali ndani ya group. Je, hiyo sheria mliyoitunga imejua na hiyo kwamba imo huo au haimo?

Je, kama haimo na hairuhusiwi mnafanya nini ili sheria i-accommodate ili kuwaepusha wanaotumia huo mtandao wasije kupatwa na matatizo ya kuhukumiwa na hiyo Sheria ya kuwa na Nyaraka za Serikali kwa sehemu zisizo husika. (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janejelly James Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria inayosimamia nyaraka za Serikali inaelekeza wazi kwamba mawasiliano ya Serikalini yafanyike kwa njia ya barua lakini haielekezi vinginevyo. Kwa hiyo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Bunge lako kwamba haitokuwa sawa na ni marufuku ya Serikali kuwasilisha au kutumiana document za Kiserikali kupitia njia ya WhatsApp na njia nyingine zisizo rasmi isipokuwa kwa yale maelekezo ambayo yatakuwa yametolewa vinginevyo katika mamlaka.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, lini Serikali itarekebisha Sheria za Utumishi zilizopitwa na wakati hasa kipindi hiki cha teknolojia?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa swali la nyongeza.

Kutokana na jibu la msingi ambalo Mheshimiwa Waziri umelitoa hauoni kwamba bado tutakuwa nyuma ya teknolojia kwa sababu mwisho wa siku tunahitaji kuweka mifumo ambayo itazilinda hizo document lakini ziende kwa haraka kwa sababu teknolojia inasaidia kufanya kazi kwa haraka?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati najibu swali la msingi nimeeleza mpaka sasa baada ya kupitishwa kwa Sheria Namba Kumi ya mwaka 2019 Serikali imekwisha tengeneza au kujenga mifumo ya TEHAMA zaidi ya 860 kwa ajili ya kusimamia utendaji wa Serikali. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mwakagenda kwamba Serikali bado inaendelea kuitengeneza mifumo mbalimbali itakayosimamia ambayo italeta Serikali yote katika adabu ya kiutendaji.

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, lini Serikali itarekebisha Sheria za Utumishi zilizopitwa na wakati hasa kipindi hiki cha teknolojia?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hii Wizara ndiyo inahusika na masuala ya TASAF watu wangu wa Jimbo la Bunda kumekuwa na matatizo makubwa sana ya malipo ya TASAF karibu nchi nzima, naomba Waziri atamke kwamba kuna nini kinachoendelea katika TASAF?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Getere, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Getere najua swali lake linatokana na ukweli kwamba yako baadhi ya matatizo au changamoto zilizojitokeza katika utendaji ndani ya Taasisi yetu inayosimamia Mfuko wa Kunusuru Kaya Maskini yaani TASAF.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba yako maamuzi na maelekezo makubwa yaliyokwishafanyika ambayo sasa yale mapungufu yote yaliyojitokeza au mapungufu kwa asilimia kubwa yaliyojitokeza ndani ya TASAF tunaweka sawa. Nataka nimhakikishie kwamba yeye na Wabunge wote humu ndani wasiwe na wasiwasi Serikali iko kazini na kazi ya kurekebisha zile kasoro zote zinaendelea kufanyika, ahsante sana.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, lini Serikali itarekebisha Sheria za Utumishi zilizopitwa na wakati hasa kipindi hiki cha teknolojia?

Supplementary Question 4

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa, Sheria ya Utumishi inaelekeza pia likizo ni haki ya mtumishi lakini likizo ile inatakiwa iambatane na stahiki zake za usafiri au nauli kwa mtumishi, lakini mpaka sasa kuna changamoto ya Walimu kupewa likizo lakini kutokupewa nauli ya kwenda makwao. Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na jambo hilo?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Kisangi, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Serikali imekuwa inapokea malalamiko ya watumishi juu ya baadhi ya madai au malimbikizo ya madai kama ambavyo ameeleza Mheshimiwa Mbunge lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali imeendelea kufanya hatua za malipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe taarifa mbele ya Bunge lako kwamba hadi sasa tunapozungumza Serikali imekwishalipa zaidi ya wafanyakazi 126,924 ambao kwa gharama ya kifedha ni sawasawa na bilioni 216 kwenda kulipa madeni yote ambayo yanaendelea, ninachoweza kusema katika Bunge lako wale wafanyakazi wote ambao wana madeni ya malimbikizo wawasiliane na Ofisi zetu kupitia Wakurugenzi wa Halmashauri pia kupitia Ofisi ya Rais ili madeni yao yote au madai yao yote ya malimbikizo tuweze kuyaangalia mara mara moja.