Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Polisi kwenye Kata za Mkiwa, Misughaa na Mungaa pamoja na nyumba za kuishi askari Singida Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Swali la kwanza; kwa kuwa ukuaji wa shughuli za kiuchumi unaongeza changamoto za kiusalama katika maeneo yetu na kwa kuwa tulikubaliana kuwa na Polisi Kata, Polisi Kata ambao hawana vituo itakuwa ni sawa na bure. Ni nini mkakati wa Serikali sasa kujenga Vituo hivi vya Polisi katika maeneo ya pembezoni, ikiwemo Mkiwa na Misughaa pamoja na Mungaa ili kuweza kusaidia ulinzi na kwa sababu wananchi wameshafyatua matofali 1000 katika Kata ya Mkiwa na mimi kwenye Mfuko wa Jimbo nimeanza kuwaunga mkono. Ni nini Serikali itafanya kwa ajili ya kutusaidia kumalizia ujenzi huo? (Makofi)

Swali la pili; Askari wetu wanafanya kazi nzuri sana na maeneo mengi hawana nyumba za kuishi, wanakaa mtaani. Ni nini mkakati wa Serikali hususan kwenye Wilaya ya Ikungi, ambayo hatuna nyumba hata moja ya Askari, hata Mkuu wa Polisi Wilaya anaishi mtaani.

Ni nini mkakati wa Serikali kuwajengea makazi Polisi wetu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali, tunapongeza sana juhudi za Mheshimiwa Mbunge lakini na wananchi wa Jimbo kwa kuanzisha ujenzi wa Vituo hivi vya Polisi katika Kata hizo ambazo amezitaja. Mkakati wa Serikali ni kuhakikisha tunaunga mkono juhudi za wananchi ili kuhakikisha tunakamilisha ujenzi huo. Katika hili tuwasiliane na Wizara ili kuhakikisha tunakamilisha majengo hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja na wameanza kufanya kazi kwa ajili ya kujenga na kukamilisha vituo hivyo vya Polisi Kata. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, moja ya mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuimarisha ulinzi na usalama ni kuona Askari wanaishi katika maeneo stahiki na yenye tija au hali nzuri katika maeneo ya kazi. Kwa hiyo, moja ya maeneo ambayo inaangalia ni kujenga nyumba za Askari katika maeneo yote ikiwemo katika Kata hii. Kwa hiyo, katika mipango ya Serikali ni kuona tunaendelea kujenga makazi ya Askari Polisi na Watumishi wengine ambao wanastahili kupata nyumba hizo ili waweze kufanya kazi zao kwa ubora zaidi. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Polisi kwenye Kata za Mkiwa, Misughaa na Mungaa pamoja na nyumba za kuishi askari Singida Mashariki?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.

Kwa kuwa, Kituo cha Polisi cha Nyang’hwale hakina hadhi na ni kidogo na kimechakaa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi cha kisasa cha Wilaya hapo Nyang’hwale?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ni kweli maeneo mengi vituo vya Polisi ikiwemo hiki cha Nyang’hwale ni vya muda mrefu, kwa hiyo vimechakaa. Kama nilivosema, moja ya maeneo ambayo Serikali tunaweka mkazo ni kuboresha vituo hivi vya Polisi, hicho ni mojawapo ya Kituo cha Polisi ambacho tutaangalia namna ya kukirekebisha, kukarabati kadri ambavyo fedha zitapatikana. Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Polisi kwenye Kata za Mkiwa, Misughaa na Mungaa pamoja na nyumba za kuishi askari Singida Mashariki?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za Askari Wilaya ya Itilima, Mkoa wa Simiyu?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo umesema ni kweli Serikali inajua umuhimu wa kuwa na vituo hivi vya Polisi, kwa hiyo, katika bajeti zake tutaendelea kutenga fedha ili kuhakikisha maeneo haya yote yanajengewa vituo vya Polisi, kadri ya muda utakavyohitajika. Nakushukuru sana. (Makofi)