Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Supplementary Question 1

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nampongeza sana Waziri kwa majibu yake mazuri sana, Mwenyezi Mungu awawezeshe ila nina maswali mawili ya nyongeza.

Moja, hiyo mobile app ambayo iko asilimia 90 itakamilika lini ili kupunguza vifo vya wavuvi ambao wanakwenda kutafuta bila kujua wanatafuta nini na wapi? (Makofi)

Swali la Pili; hivi Serikali ilishawaeleza wavuvi wajibu wao kuhusiana na mobile app ambayo wanaingeneza? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y. WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amour Khamis Mbarouk, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye majibu yangu ya msingi kwamba, hii application tayari imekwishakamilika, iko katika asilimia 90. Asilimia 10 hiyo ni ile ya kuangalia ule mfumo unaweza kufanya kazi kwa usahihi kiasi gani. Halafu, hatua ya pili itakuwa inajibu swali lake la pili kwamba, wavuvi kama wamekwishakujulishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mfumo huu kuwa umekamilika, tutaanza hatua ya kuwajulisha wavuvi wote ili kuweza kunufaika na utaratibu huo, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wavuvi katika makundi mbalimbali. Ahsante.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, wakati wa hotuba ya Bajeti Kuu mwaka 2023/2024, Bunge hili lilipitisha Tozo ya shilingi 100 kwa kila kilo moja ya samaki wakavu aina ya dagaa wanaosafirishwa kuingia nchini au Kwenda nje ya nchi. Jambo hili limetafsiriwa vibaya Jimboni Ukerewe, jambo ambalo limefanya watumishi wanatoza wananchi shilingi 100 kwa samaki wanaosafirishwa ndani ya Wilaya jambo ambalo limeleta taharuki kubwa Jimboni Ukerewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninataka kupata kauli ya Serikali juu ya jambo hili ili kujenga amani kwa wananchi wa Jimbo la Ukerewe. Nashukuru. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze, jambo hili amekuwa akilifuatilia sana kwenye Wizara ili kuhakikisha wavuvi waliopo katika ukanda huo wa Ziwa Victoria na pale Ukerewe wananufaika zaidi na biashara wanayoifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha marekebisha ya tozo, awali tozo ilikuwa kuanzia kilo 0 - 500 ilikuwa haitozwi chochote, lakini kilogramu kuanzia 501 na kuendelea ilikuwa inatozwa shilingi 100. Kwa kuzingatia kwamba ile ni biashara ya ndani na nje (import and export business) haiwezi kuwa na masharti sawa na ufanyaji wa biashara ndani ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ni kosa la kitafsiri la kanuni na sheria, hivyo natumia fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi kumwagiza Katibu Mkuu awasiliane na Mheshimiwa Mbunge ili kwenda kurekebisha changamoto hiyo inayowapata wavuvi wa hapo Ukerewe, ahsante. (Makofi)

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza; je, Serikali ipo tayari kugawa vifaa kwa wavuvi ili waweze kutumia hiyo mobile app? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Mwinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza tangu awali kwenye majibu yangu ya msingi kwamba Serikali tupo tayari, ilikuwa kwanza ni kuangalia namna gani tunaweza tukawafanya wavuvi wetu waweze kunufaika na mazao ya bahari au mito na maziwa kwa kufanya huo utafiti na kupata hiyo application ambayo ni maalum inayosaidia wao kuweza kujua mazalia ya samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, huu mpango ni pamoja na utaratibu wa kuweza kuwafundisha, kuwapa elimu, na pia utaenda sambamba na kuwapa vifaa. Zaidi hapa watatumia simu zao za mkononi tu kuweza kujua mazalia ya samaki na kupata taarifa zaidi. Kwa hiyo, tutaendelea kushirikiana nao na kuwawezesha kiutaalamu, kielimu, na kiujuzi katika kuhakikisha kwamba tunapata tija iliyokusudiwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kukuza sekta ya uvuvi. (Makofi)

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Supplementary Question 4

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tatizo linalowakumba wavuvi wetu nchini ni kukosa zana bora za uvuvi. Serikali katika bajeti yake ilisema itanunua meli za uvuvi ili igawe, ipeleke katika sehemu mbalimbali. Nataka kujua, mkakati huo umefikia hatua gani? Kwa sababu Mtwara kule sisi hatujapata hiyo meli. (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika bajeti ilielezwa, lakini pia tumeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuwasiliana kwanza kwenye masuala ya fedha, kuhakikisha tunapata fedha na kutekeleza bajeti kwa kadri ilivyokuwa imepangwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024. Hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, yale yote ambayo tuliyapitisha katika bajeti, tupo kwenye hatua za utekelezaji na tutahakikisha kwamba tunayatekeleza kama ambavyo tumekuwa na matamanio, likiwemo hilo la kuweza kununua meli na kuboresha katika sekta hiyo ya uvuvi kwa kuleta mitambo ya kisasa na pia kutumia teknolojia ya kisasa, ahsante. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawaendeleza wavuvi kwa kuanzisha uvuvi unaotumia dira maalum inayoelekeza samaki walipo?

Supplementary Question 5

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Ni lini Serikali itapunguza tozo ya shilingi 7,000 ambayo wavuvi wanatozwa wanapoingia kuvua samaki mle ndani ya Ziwa Rukwa? Ni lini sasa Serikali itakuja kupunguza tozo hiyo? Ahsante.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la lini Serikali itapunguza tozo, kwanza ni kupata uhakika wa aina ya tozo na kiwango kinachotozwa kwenye maeneo hayo. Kwa hiyo, naomba suala hili nilichukue kwa sababu linahusiana zaidi na takwimu ili kuweza kupata uhakika kwanza wa tozo zinazotozwa, na pili, kuweza kuona utaratibu wa kisera pamoja na kanuni na sheria zinasemaje katika eneo hilo na hatua ya tatu itakuwa ni kuleta mapendekezo ya kuona unafuu utapatikanaje kwa wavuvi wetu ili waweze kupata faida zaidi, ahsante. (Makofi)