Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO K.n.y. MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza ujenzi wa Kituo cha Polisi Turiani kilichojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na tunakupongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu hayo na tunatarajia kwamba wana Mvomero watapata huduma hiyo mara moja baada ya ushirikiano kutoka Serikali Kuu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza; swali la kwanza, je, ni lini sasa mradi huu utaanza kupewa support na Serikali ili kuonesha jitihada za wananchi wa Mvomero walizozianzisha?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nakumbuka mwezi Julai Mheshimiwa Naibu Waziri ulitembelea katika Jimbo la Kishapu na Wilaya ya Kishapu, ukaona jitihada za ujenzi wa Ofisi ya OCD pale Kishapu; na jumla ya shilingi milioni 275 zinahitajika kwa ajili ya kukamilisha mradi huo; na uliahidi utapeleka fedha hizo kuhakikisha kwamba mradi huo unakamilika;

Je, ni lini fedha hizi zitafika ili ukamilishaji wa mradi huo wa Ofisi ya OCD uweze kukamilika? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusu hili la mradi wa ujenzi wa kituo kule Mvomero, ni ahadi yetu kwamba katika mwaka wa fedha 2024/2025 kituo hiki kimeingizwa kwenye mpango na fedha zinazopungua zaidi ya shilingi milioni 60 zitatolewa na Jeshi la Polisi ili mradi huo utekelezwe na kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Kishapu, kwanza nawapongeza wananchi waliojitolea pamoja na Halmashauri yao na Mheshimiwa Mbunge kujenga kituo bora kabisa, kinachohitaji ni umaliziaji. Tumeahidi, katika bajeti ya mwaka huu zimetengwa shilingi milioni 275 kwa ajili ya ukamilishaji huo.

Mheshimiwa Spika, kupitia Bunge hili nimhimize IGP kuhakikisha kwamba anapeleka fedha hizi mapema iwezekanavyo ili ukamilishaji ule ufanyike na hatimaye huduma za kipolisi ngazi ya Wilaya ziweze kutolewa, ahsante.