Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza:- Je lini maji safi na salama yatapelekwa katika Kata za Kiegei, Kilimarondo, Matekwe na Namapwia – Nachingwea?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Mji wa Nachingwea ni mji unaokua haraka sana. Upo Mradi wa Maji pale Nachingwea ambao tayari sasa hivi imeonekana mradi ule hautoshelezi. Je, Serikali iko tayari kutupatia fedha Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea ili kupanua Mradi ule wa Maji wa Mji wa Nachingwea?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kama ilivyo kwa Mji wa Nachingwea unakua haraka, Mji wa Liwale nao una mradi sasa una miaka zaidi ya miwili kwa ajili ya maji katika Mji wa Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutupatia fedha ili tuondokane na adha ya maji pale Mjini Liwale? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amandus, kwa niaba yake yameulizwa na Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu pesa Nachingwea kwa ajili ya kupanua mradi; nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, hili tunalifanyia kazi. Tayari lipo kwenye mipango kuhakikisha katika Mji wa Nachingwea wanapata huduma ya majisafi na salama na ya kutosheleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pesa Liwale, nimelipokea, tutalifanyia kazi. Pia naomba kumpa taarifa, wale wawekezaji wetu walishafika Liwale, naamini atakuwa amewaona, watakwenda kufanya usambazaji wa visima vilivyochimbwa. Yote hii ni kuona kwamba jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kumtua mama ndoo kichwani Liwale nazo zinaweza kukamilika.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA K.n.y. MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza:- Je lini maji safi na salama yatapelekwa katika Kata za Kiegei, Kilimarondo, Matekwe na Namapwia – Nachingwea?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika Mji wa Kasulu eneo la Mwilamvya kuna tatizo la upatikanaji wa maji. Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la maji katika Mji wa Kasulu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Genzabuke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo ya Kasulu tayari pia tuna mipango ya kuona kwamba tunakuja kuongeza huduma ya maji. Mwaka huu wa fedha tutafanya kazi kubwa sana Kasulu kuhakikisha maeneo ambayo maji hayajafika yaweze kupatikana.