Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupunguza upoteaji wa Uoto wa Asili nchini unaosababisha kupoteza hadhi kwa Hifadhi na Mapori ya Akiba?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Hifadhi za Taifa, Hifadhi za Misitu pamoja na Mapori ya Akiba, tumeanzisha kwa ajili ya kuhifadhi uoto wa asili na kulinda viumbe hai pamoja na wale ambao wako hatarini kutoweka. Hali kadhalika kwa kuwa hivi karibuni maeneo mengi ya hifadhi na mapori ya akiba, aidha tumeyamega ya kuyateremsha hadhi baadhi yake. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba utaratibu huu wa kumega maeneo na kuteremsha hadhi maeneno ya hifadhi haujirudii tena?

Swali la Pili, kwa kuwa upoteaji wa uoto wa asili unaenda sambamba na upoteaji wa viumbehai, mimea na wanyama ambao wako hatarini kutoweka. Je, Serikali ina mpango gani wa kuainisha na kuwea kutenga utaratibu maalum wa kuweza kuhifadhi viumbe adimu na wale ambao wako hatarini kutoweka? Ahsante sana.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iliridhia kuachia maeneo yenye migogoro vilevile kushusha hadhi baadhi ya mapori na hifadhi zetu baada ya kubaini kwamba ipo migogoro isiyokuwa na tija iliyokuwa inahatarisha usalama wa wananchi wetu. Serikali ilifanya hivyo baada ya kufanya utafiti wa kina kuona kiasi cha matumizi endelevu ya maeneo hayo, jinsi ambavyo yanaweza kutumika na kama yalikuwa yanatumika kwa jinsi ambavyo ilivyokuwa imekusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pale inapoonekana kwamba pori au hifadhi imepoteza sifa yake ya awali ya msingi, basi maeneno hayo hushushwa hadhi na kuwa misitu ili tuweze kuendelea kutunza maeneno haya. Katika kujipanga kuhakikisha kwamba hali hii haijitokezi tena, Serikali inajipanga kutoa elimu kwenye maeneo yote yanayozunguka maeneo ya hifadhi zetu na mapori tengefu ili kujenga uelewa wa wananchi kuhusiana na umuhimu wa rasilimali hizi, vilevile Serikali imejipanga kuongeza doria katika maeneo haya ili uvamizi usijitokeze tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, Serikali inajitahidi sana kuhakikisha kwamba pale ambapo mimea imetoweka au wanyama wametoweka Serikali imekuja na mkakati wa kupanda miti kwenye maeneo yale yaliyoathirika, kwa mfano kupitia TFS tumeaza kupanda miti kule Mkoani Geita, vilevile tumeanza kupanda miti Mkoani Kigoma zaidi ya hekta 139,000 zimepandwa ili kuhakikisha uoto ule haupotei.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pale ambapo tunaona kwamba kuna aina fulani ya wanyama inatoweka, tunakuwa na mkakati wa kuweka maeneo maalum ya kuhakikisha tunadhibiti kuzaliana kwa wanyama wale ili wasije wakatoweka. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MOHAMED JUMAH SOUD aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupunguza upoteaji wa Uoto wa Asili nchini unaosababisha kupoteza hadhi kwa Hifadhi na Mapori ya Akiba?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Hifadhi ya Msitu wa Kihesa - Kilolo pia imekutana na athari hizo. Je, Serikali iko tayari kutusaidia na sisi kuja kupanda miti ili kuendela kuhifadhi eneo lile?

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, tumelichukua, wataalam wetu wataenda kufanya tathmini na kuona jinsi ambavyo tunaweza kusaidia.