Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza:- Je, lini Vijiji vya Namikunda, Chipole, Machombe, Mtakateni, Machenje, Matawale, Mpekeso, Chakama na Kata ya Temeke vitapewa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, tuna Kijiji cha Mlundelunde, Kitongoji cha Mchaka ambacho kina shule ya sekondari ambapo bahati mbaya umeme umepita juu yake na shule ile ya sekondari kama taasisi ya Serikali, haijapata ule umeme: Je, nini maelekezo ya Serikali kwa REA Mtwara ili waweze kufanya haraka kuunganisha umeme katika hiyo shule ya sekondari?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Tumepata changamoto kubwa kwa Jimbo letu la Masasi Mjini ambapo tuna Kata saba za Sururu, Mwengemtapika, Matawale, Chanikanguo, Temeke, Marika pamoja na Mmbaka ambazo ziko vijijini, lakini wanatakiwa kulipa shilingi 320,000/= kama sehemu ya ada ya uunganishaji wa umeme: Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa, wananchi hawa wapate haki kwa maana wapo vijijini, waunganishiwe umeme kwa shilingi 27,000/= kama vijiji vingine?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Geoffrey Mwambe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na shule ambayo ameitaja, shule hii ipo katika moja ya kitongoji ambapo utaenda kutekelezwa mradi wa vitongoji 15 ambavyo tayari Serikali imeshatenga fedha kwa mwaka huu wa fedha. Tunaanza kufanya ufuatiliaji ili tuweze kuona ni namna gani tunaanza kutekeleza mradi huu wa vitongoji 15.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la pili juu ya maeneo ya vijijini ambayo yanakataliwa kutozwa shilingi 27,000/=, tayari Serikali tumeshaya-identify haya maeneo na tuko katika mchakato wa mwisho ili kuweza kutolea maelekezo kwa maeneo kama haya ambayo yanaleta mkanganyiko wa bei.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza:- Je, lini Vijiji vya Namikunda, Chipole, Machombe, Mtakateni, Machenje, Matawale, Mpekeso, Chakama na Kata ya Temeke vitapewa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Mkandarasi aliyekabidhiwa vijiji 15 vya Wilaya ya Hanang’ kasi yake inasuasua sana: Je, nini kauli ya Serikali juu ya Mkandarasi huyu ili kuwapa matumaini wananchi wa Wilaya ya Hanang’?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halamga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkandarasi aliyekuwepo Hanang’ Nakurwa Investment Company ni kweli alikuwa anasuasua lakini tumemsimamia na katika vijiji 15 ambavyo vimebakia, vijiji tisa ameshasambaza nguzo, na tuna imani mpaka ifikapo Desemba, 2023 atakuwa amekamilisha kuweka umeme vijiji vyote, ahsante.