Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, lini Serikali itafungua Ofisi za Balozi katika nchi za Iran na Pakistan?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, Nchi ya Iran ina miaka 56 ya ubalozi hapa nchini, lakini nchi ya Pakistani ina miaka 40 ya ubalozi hapa nchini.

Je, Serikali haioni muhali kidiplomasia kwa miaka yote hii kutokufungua ubalozi kwenye nchi hizi mbili?

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine, swali la pili, kama nilivyosema kwa wingi wa miaka ya balozi hizi ambazo ziko hapa kwetu nchini na Serikali kwa kufanya tathmini kwa miaka 56 na miaka 40. Je, commitment yake ni lini sasa itafungua balozi kwenye nchi hizi mbili?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na kwamba, nchi yetu haina ofisi za ubalozi nchini Pakistan na Iran, lakini hata hivyo tumekuwa na ushirikiano mkubwa na tumekuwa tukishirikiana katika nyanja mbalimbali. Tuna mikakati mingi ya kuendeleza uhusiano huu na mmojawapo ni kuanzisha tume za pamoja za kudumu za ushirikiano kati ya Tanzania na Pakistan na Tanzania na Iran. Kwa Iran tayari hiyo ipo na kwa Pakistan tayari tumeshaanza mchakato huo na tayari tumewasilisha rasimu ya makubaliano hayo na ipo upande wa Ubalozi wa Pakistan tukisubiri majibu yao.

Mheshimiwa Spika, lingine, nchi yetu inapenda kuwa na balozi nyingi sana nchi za nje, lakini ni muhimu sana kufanya tathmini, kama nilivyoeleza hapo mwanzo, ili kujua tija hasa ambazo tutapata katika nchi hizo. Pia hali ya kifedha inaporuhusu nafungua hizo balozi. Nakushukuru sana. (Makofi)