Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi kwa kumalizia ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto, Lupa?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na naishukuru Serikali kwa majibu mazuri na tunaona namna ambavyo wanatuunga mkono na sisi tunasema ahsante. Tunaiomba tu Serikali tuweze kupata hizi fedha kwa wakati ili hivi Vituo vya Polisi viweze kukamilika.

Nina maswali mawili madogo ya nyongeza; Kituo cha Polisi cha Chunya Mjini ni Kituo cha Polisi cha zamani toka ukoloni, kidogo na kiko ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya; je, ni upi mpango wa Serikali kuwezesha kujengwa kituo kikubwa cha Polisi chenye hadhi ya wilaya katika Wilaya yetu ya Chunya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Wilaya ya Chunya ina changamoto kubwa ya nyumba za askari; je, ni upi mpango wa Serikali kuweza kujenga nyumba za askari ili waondokane kuishi katika mazingira magumu katika Wilaya ya Chunya? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni mpango wa Wizara kupitia Jeshi la Polisi kuhakikisha kwamba Wilaya zote nchini zinapata vituo vyenye hadhi ya Wilaya ambavyo vitakuwa na OCD, OC-CID, askari wa idara nyingine na askari wa kawaida ili kuwezesha ulinzi wa raia na mali zao. Nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira ya Serikali kulitekeleza hili bado ipo na nikuahidi kwamba katika mpango wake wa miaka 10 ambapo sasa hivi miaka miwili imepita ya ujenzi wa vituo hivi, tutahakikisha kituo cha wilaya yako kinaingia katika mpango angalau mwaka ujao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu nyumba tumwombe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunapojenga Kituo cha Polisi cha ngazi ya Wilaya au vituo vya Polisi daraja C ngazi ya kata na tarafa, tuhakikishe eneo linakuwa kubwa la kutosha kwa ajili ya kujenga kituo pia na makazi ya askari na viongozi wao. Kwa hiyo, wilaya ikituhakikishia uwepo wa viwanja hivyo tutaingiza kwenye mpango wa ujenzi wa kituo pamoja na nyumba, ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi kwa kumalizia ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto, Lupa?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, katika Mji wa Njombe tuna Kituo cha Polisi ambacho hakina hadhi ya makao makuu ya mkoa; je, ni lini kituo chenye hadhi ya mkoa kitajengwa katika Halmashauri ya Mji wa Njombe? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba mikoa yote ambayo haina vituo vya ngazi ya mkoa, vinajengewa vituo hivyo. Tumeanza kwa awamu katika maeneo mengine na Njombe ni eneo lingine ambalo litapewa kipaumbele katika mwaka ujao wa fedha, kuanza kujenga Kituo cha Polisi ngazi ya mkoa, nashukuru. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi kwa kumalizia ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto, Lupa?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Gereza la Wilaya ya Nyang’hwale kwa sababu huduma hiyo tunaipata kwa umbali mrefu sana zaidi ya kilometa 100? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, japo swali ni la polisi, lakini nakubali tu kwamba ni nia ya Serikali kadri huduma za magereza zinapokuwa mbali zinaongeza gharama za kusafirisha washtakiwa au mahabusu kutoa eneo lile kwenda enei lingine ambapo bado inakuwa ni sehemu ya gharama za Serikali. Nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu nina ahadi ya kutembelea Jimbo lake la Nyang’hwale tutajiridhisha kuona eneo kama lipo la kutoa ili Jeshi la Magereza liingize katika mpango wake wa ujenzi, nashukuru. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi kwa kumalizia ujenzi wa Vituo vya Polisi vya Itumbi na Kambikatoto, Lupa?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nami niulize swali dogo la nyongeza. Waziri unacheka kwa sababu unajua ninachouliza.

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Polisi Bunda hakina hadhi ya Wilaya na kinahudumia majimbo matatu; ni lini sasa mtatuhakikishia mnatujengea kituo chenye hadhi ya Wilaya na hii ni zaidi ya mara kumi nakuuliza wewe hapo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, swali analoliuliza Mheshimiwa Bulaya najua kwamba Mbunge wa Jimbo ameshaniuliza mara kadhaa pia. Namuahidi tu kwamba pale Bunda eneo kilipo Kituo cha Polisi ni eneo dogo, limebanwa na barabara, kupitia jukwaa hili, nauomba uongozi wa Wilaya ya Bunda wapate eneo la kutosha kwa ajili ya kuweka mpango wa ujenzi wa Kituo cha Polisi cha hadhi ya Wilaya, nashukuru sana. (Makofi)