Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Mtitaa Wilayani Bahi?

Supplementary Question 1

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bwawa la Chikopelo linategemewa na Kata za Chali na Kata ya Nondwa. Bwawa hili limekuwa na uwezo wa kutunza maji msimu wote, hata hivyo lina changamoto ya kupungua kwa kina kutokana na kujaa kwa matope.

Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati bwawa hili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine dogo ni kwamba Kilimo cha Zabibu ni kilimo kinachotegemewa hapa Mkoa wa Dodoma hata hivyo kilimo hiki bado kinategemea kwa kiasi kikubwa mvua. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka utaratibu ili tuanze kupata umwagiliaji kwa ajili ya kilimo na kupata tija? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza kuhusu Bwawa la Chikopelo. Katika hotuba ya bajeti ya Wizara ya Kilimo kiambatisho namba 13 tumelitamka Bwawa la Chikopelo kati ya mabwawa ambayo tunakwenda kuyafanyia kazi mwaka ujao wa fedha. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na Kata za Nondwa alizozitaja na maeneo ya jirani kuwa bwawa hili linakwenda kufanya kazi na wananchi watanufaika kwa kilimo cha umwagiliaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu zabibu, tunatambua kwamba Dodoma ni kati ya eneo ambalo lina uzalishaji mkubwa sana wa zabibu hapa Tanzania na hivyo kuna umuhimu pia wa kuunganisha zao hili na kilimo cha umwagiliaji. Kwa kuanzia tunao tayari mfumo wa umwagiliaji katika eneo letu la Chinangali ambapo tunalo shamba kubwa la umwagiliaji kwa ajili ya kilimo cha zabibu. Sambamba na hilo hata hili Bwawa la Chikopelo pia na lenyewe tutaangalia ikolojia yake kama ita-support kilimo cha zabibu pia tutaunganisha mifumo hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni kwamba tumetamka hapa tunakwenda kuchimba visima 150 kila Halmashauri nchi nzima hivyo wakulima wa bahi pia watanufaika na visima hivi kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji cha zabibu.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Mtitaa Wilayani Bahi?

Supplementary Question 2

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa na mii swali la nyongeza. Je, Serikali imefikia wapi kwenye ujenzi wa Skimu za Umwagiliaji Wilayani Mbarali? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tumekuwa na miradi ya umwagiliaji katika Wilaya ya Mbarali na ninavyozungumza hivi sasa Wakandarasi wapo site katika mradi wa Msesule, Isenyela, Matebete, Hemanichosi na Gwanakubagogolo kote huko tayari wakandarasi wako site na kazi inaendea. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba kazi inaendelea na wananchi watanufaika na kilimo cha umwagiliaji.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Mtitaa Wilayani Bahi?

Supplementary Question 3

MHE. SYLIVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Mkoa wa Kigoma ni kati ya Mikoa iliyobarikiwa kuwa na vyanzo vikubwa vya maji lakini bado suala la umwagiliaji halijapewa kipaumbele. Nataka kujua, wananchi wa Kasulu, Buhigwe na Uvinza ni lini watanufaika na miradi hii ya umwagiliaji? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba yetu ya bajeti kiambatisho namba tano tumeyatamka mabonde 22 ambayo tunakwenda kuyafanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya umwagiliaji. Bonde mojawapo ni Bonde la Mto Malagarasi ambalo lina hekta 7000 na litahudumia eneo la Buhigwe, Kasulu pamoja na Uvinza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo katika eneo la Kasulu tuna miradi miwili pale ambayo tunaifanyia kazi katika mwaka ujao wa fedha mradi wa Ahsante Nyerere na Kilimo Kwanza ambayo ina jumla ya hekta 3,500 ipo ndani ya mpango itafanyiwa kazi na wakulima wa Kigoma watafanya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. KENNETH E. NOLLO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Mtitaa Wilayani Bahi?

Supplementary Question 4

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba niulize swali moja dogo la nyongeza.

Ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuwapatia skimu ya umwagiliaji watu wa Mkinga?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba lazima tufanye kilimo cha umwagiliaji ili tuweze kuleta tija kwenye kilimo. Katika eneo la Mkinga pamoja na Lushoto tumeanza kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa bonde la Mto Umba ambalo lina hekta zaidi ya 5,560 na tunaamini kabisa kwamba wananchi wa eneo la Mkinga watanufaika na mradi huu mkubwa ambao unakuja kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.