Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itawasaidia Wananchi wa Mtwara Mjini waliojiunga na PRIDE kurejeshewa fedha zao?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mwaka jana Mheshimiwa Waziri aliahidi kuja Mtwara kuzungumza na wadeni hao. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuja Mtwara kuja kuzungumza na hawa ambao wana wadai? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; wananchi wa Jimbo la Mtwara wameahidiwa mara kwa mara juu ya majibu ya Mheshimiwa Waziri. Sasa ni lini sasa mtakuja kuwapa fedha zao hao wananchi wa Mtwara?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hassan Mtenga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mimi niko tayari kabisa kwenda kuwasikiliza na kukaa na wananchi wa Mtwara Mjini kuhusu madai yao mara tu baada ya Bunge kumalizika tutakaa na Mheshimiwa Mtenga tuende kukutana na wananchi hao.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba taratibu za ufilisi zinaendelea na kuanzia Julai mwaka wa fedha unaokuja tunaenda kuwalipa wananchi kwa mujibu wa sheria. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itawasaidia Wananchi wa Mtwara Mjini waliojiunga na PRIDE kurejeshewa fedha zao?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa, kumekuwa na taarifa kwa wachuuzi wadogo wadogo maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Wilaya ya Nyang’hwale, kwa kupungukiwa na silver ama sarafu ndogo ndogo kuanzia shilingi 50, 100, 200 na 500 na kusababisha mfumuko wa bei kwenye masoko yetu madogo madogo.

Je, Wizara inalitambua hilo? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amar, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ninamuomba tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hili tulichukue tukalifanyie kazi, tukafuatilie tuone kwamba hivyo ndivyo hali halisi ilivyo na tuone ni njia gani ya kulipatia utatuzi suala hilo. (Makofi)

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itawasaidia Wananchi wa Mtwara Mjini waliojiunga na PRIDE kurejeshewa fedha zao?

Supplementary Question 3

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kusimamia taasisi ndogondogo zinazoumiza wananchi katika mikopo yake kama hizi zinazojulikana kama kausha damu, komandoo, rusha roho na kadhalika? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango na mikakati na ndiyo maana tumeanzisha sheria na taratibu kwa hiyo taasisi yoyote ambayo inaanzisha mikopo lazima ifuate sheria na taratibu na iwe imesajiliwa na Benki Kuu ya Tanzania. (Makofi)

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, lini Serikali itawasaidia Wananchi wa Mtwara Mjini waliojiunga na PRIDE kurejeshewa fedha zao?

Supplementary Question 4

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Yaliyotokea Mtwara Mjini kwa PRIDE pia yametokea ndani ya Iringa Manispaa. Je, zoezi hilo Julai mtalifanya kwa wote nchi nzima pamoja na Iringa Manispaa walioathirika?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jesca kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tuliposema kwamba Kampuni hii ya PRIDE tayari imefanyiwa taratibu na Sheria ya Ufilisi, tunaenda kulipa fedha hiyo kwa wadai walioko Mtwara nina maana kwamba ni nchi nzima wale ambao wana madai Julai tutaanza kulipa fedha hiyo. (Makofi)