Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bungu hadi Nyamisati Wilaya Kibiti?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali: Je, mko yatari kuanza sasa usanifu na ujenzi wa barabara hiyo kwenye bajeti ya mwaka huu unaokuja Julai, 2023/2024?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Alice Kaijage, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika jibu langu la msingi, nilisema tunakamilisha usanifu wa kina mwezi huu tarehe 30 Juni. Tayari bajeti imeshapitishwa. Kwa hiyo, hiyo barabara itaingizwa kwenye mpango wa mwaka unaofuata kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bungu hadi Nyamisati Wilaya Kibiti?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyonyeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kuanzia Gairo – Chanjale - Kibakwe hadi Mpwapwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hii barabara ilifanyiwa usanifu wa awali na bado haijafanyiwa usanifu wa kina. Kwa hiyo, barabara hii ikishafanyiwa usanifu wa kina, Serikali itakuwa imefahamu gharama ya hiyo barabara na ndiyo tutaanza sasa kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bungu hadi Nyamisati Wilaya Kibiti?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya Bungu - Nyamisaki ni barabara ya muda mrefu sana kabla hata bandari haijajengwa. Tumeuliza haya maswali humu muda mrefu na siku nyingi na kila tukiuliza wanasema tutajenga. Tunaomba commitment ya Serikali, barabara hii mtaijenga lini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Salma Kikwete Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ni ya siku nyingi na tunatambua umuhimu wake kwamba barabara hii ndiyo inayounganisha Pwani na Kisiwa cha Mafia. Commitment ya Serikali kama nilivyosema, ndiyo maana sasa tumeamua kuifanyia usanifu yakiwa ni maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, tunavyoongea, kazi inaendelea. Kwa hiyo, tuna hakika baada ya kukamilisha usanifu, barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bungu hadi Nyamisati Wilaya Kibiti?

Supplementary Question 4

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya kutoka Ifakara – Lumemo – Michenga – Idete mpaka Mlimba imeshatangazwa; je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante ni kweli kwamba barabara hiyo imeshatangazwa na nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajenga kilometa 100 na tuna lots mbili. Kinachosubiriwa sasa hivi ni kusaini mikataba na wakandarasi ambao wamepatikana kwa ajili ya kuanza ujenzi huo wa barabara, ahsante.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bungu hadi Nyamisati Wilaya Kibiti?

Supplementary Question 5

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Barabara ya Nyoni - Maguu inayopitia Mawono kwenye mlima mkali, ni lini tutaanza ujenzi kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara anayoitaja Mheshimiwa Kapinga ni kweli, na ipo kwenye ilani kwamba ijengwe kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga, lakini kitu ambacho tunategemea tukifanye kwanza ni kuhakikisha kwamba yale maeneo yote yenye miinuko tunajenga aidha kwa zege ama kwa lami nyepesi ili kupunguza changamoto kwa wasafiri ambao wanasafiri katika hiyo barabara ya Nyoni – Maguu, ahsante.